Quantcast
Channel: VIJIMAMBO
Viewing all 45987 articles
Browse latest View live

Alex King aunga mkono juhudi za Rais Magufuli

$
0
0

 Mchungaji wa huduma ya Jesus King of Kings Ministries, Alex King wa Maryland nchini Marekani akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuelezea hisia zake katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 Na Mwandishi wetu

MCHUNGAJI wa Kitanzania anayehudumu Jesus king of kings ministries, Maryland Marekani, Alex King amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika kipindi kifupi, mafanikio ambayo yanatakiwa watanzania wote kujivunia.

Aidha amesema kwamba mwaka huu alirejea nyumbani kuja kuona sifa ambazo Rais John Magufuli amekuwa akipewa jinsi alivyoliendesha taifa katika kipindi cha miaka mitano, na kusema kiongozi huyo ni zawadi ya Mungu.

"Alisema Marekani ilichukua miaka 200 kutengeneza uchumi imara kwa kuwanyonya waafrika lakini Rais Magufuli kwa miaka mitano amefungua Tanzania na kuifanya kuwa moja ya taifa linalokua kasi kiuchumi na kiimani kwa Mungu.

"Nimefurahi ujenzi mkubwa unaoendelea hapa na kwamba makandarasi wote wanalipwa, hii ni neema Marekani ilijengwa na watumwa na sasa wanatafuta fidia" alisema King.

Alisema ameamua anaporejea Marekani kuwa balozi wa hiari wa kutangaza Tanzania ili kila mtu atambue nini kinafanyika katika taifa hili lililochaguliwa na Mungu.

"Hakuna watu wa kuisemea nchi yangu vizuri huko nje, nitaisemea" alisema King.

Mtanzania huyo mwenye asili ya Singida ambaye kwa sasa ana uraia wa Marekani kupitia mfumo wa Greencard, akizungumza na waandishi wa habari jana kabla ya kurejea nchini Maryland, alisema ujenzi wa miundombinu ya barabara na hospitali yameonesha ni kwa namna gani Tanzania inasonga mbele katika kuhakikisha kwamba wananchi wake wanaishi katika neema.

"Nimefika nyumbani Singida kuna hospitali kubwa ya rufaa pale, yaani sasa wananchi hawawezi kufa kwa kukosa huduma ya rufaa" alisema King.

Akizungumzia ugonjwa wa Covid-19 alisema kwamba Mungu ameisaidia Tanzania kukabiliana na mazingira ya ugonjwa huo kutokana na kiongozi wa nchi kuwa na imani kubwa na Mungu.

"unaweza kuona yote hayo yalianza kwa Rais Magufuli kuitisha maombi ya kufunga kwa siku 3 kwa watanzania wote. Haikuwa kwa waislamu na wakristo pekee aliwaagiza hata wapagani na kuagiza waite Mungu, na tunaona nini Mungu amekitenda" alisema King na kuongeza kuwa ni kama vile Nabii Elia alivyofanya nchini Israel.

Mtumishi huyo wa Mungu amesema kwamba Tanzania inalindwa na Mungu na katika yeye ametoa taifa lenye shuhuda nyingi na mafanikio makubwa katika elimu, afya na ustawi wa jamii.

"Nimefurahi sana na uwapo wa elimu bure manake hata watu maskini wanaweza kufika Chuo kikuu ambako pia wanakopeshwa kuendesha elimu hiyo. Nimefika nyumbani na kumkuta mpwa wangu akiwa anatunukiwa digrii yake ya kwanza. Aksante sana Magufuli kuwezesha hili'" alisema King

Pamoja na kuwataka watanzania waendele kutunza jamii yao kumuogopa Mungu aliwataka kuendelea kuchapakazi kwa bidiii kwa manufaa ya taifa  na kuwasihi watanzania waliopo nje kurejesha mitaji nyumbani.

"Nimeona mambo yanayofanyika hapa nyumbani ni makubwa watanzania tuishio nje tupiganie nchi yetu turejeshe mitaji" alisema na kuongeza kwamba  wakati umefika wa Rais John Magufuli kufikiria uraia pacha ili watanzania waliopo nje wawe na uhakika na uwekezaji nyumbani.


TANGAZO LA UCHAGUZI MKUU NEW YORK

KATIBU MKUU MHANDISI ANTHONY SANGA AKUTANA NA BALOZI WA AUSTRIA NCHINI

$
0
0
Mazungumzo yakiendelea baina ya Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga na ugeni uliomtembea
Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga akifurahia jambo pamoja na Balozi wa Austria nchini Tanzania Dkt. Christian Fellner aliyefika ofisini kwake katika mji wa Serikali Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Austria nchini Tanzania Dkt. Christian Fellner, na wafanyabiashara kutoka Austria alioambatana nao
Baadhi ya wafanyabiashara walioongozana na Balozi wa Austria nchini Tanzania Dkt. Christian Fellner wakiwa ofisini kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga (hayupo pichani).

Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga amekutana na Balozi wa Austria nchini mwenye makazi yake nchini Kenya, Dkt. Christian Fellner ofisini kwake katika mji wa Serikali Dodoma.

Mhandisi Sanga amefanya mazungumzo na Balozi Christian aliyeambatana na baadhi ya wafanyabiashara wenye makampuni makubwa kutoka Austria, kwa lengo la kuangalia namna ya kushirikiana katika sekta ya maji.

“Kimsingi, tunaangalia sehemu ambazo tunaweza kushirikiana nao katika uwekezaji wa miundombinu ya maji, kupitia ugeni huo tunatafuta pesa za kujenga miradi ya maji,” Mhandisi Sanga, amesema.

Naye balozi Dkt. Christan Fellner amesema kwamba anamshukuru sana Balozi wa Tanzania nchini Kenya Balozi John Simbachawene kwa kuandaa na kuwezesha ujumbe wa wafanyabiashara hao kufika Tanzania na kufanikisha mazungumzo hayo.

Naye, Balozi Simbachawene amesema makampuni hayo 13 ya kimataifa kutoka Austria yamevutiwa katika masuala ya uwekezaji hapa nchini hususan maendeleo ya kuboresha miundombinu mbalimbali.

RAIS WA ZANZIBAR DK.HUSSEIN MWINYI AMEWAAPISHA WAKUU WA MIKOA ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi
Unguja aliyemteua hivi karibuni Mhe Idrisa Kitwana Mustafa, hafla hiyo
ya kuapishwa imefanyika leo 3/12/2020 katika ukumbi wa Ikulu Jijini
Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba
aliyemteua hivi karibuni Mhe Salama Mbarouk Khatib, hafla hiyo ya
kuapishwa imefanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha
na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja
aliyemteua hivi karibuni Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, hafla hiyo
imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 3/12/2020.(Picha
na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja
aliyemteua hivi karibuni Mhe.Rashid Hadidu Rashid, hafla hiyo ya
kuapishwa imefanyika leo 3/12 /2020 katika ukumbi wa Ikulu Jijini
Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi
Unguja aliyemteua hivi karibuni Mhe Idrisa Kitwana Mustafa, hafla hiyo
ya kuapishwa imefanyika leo 3/12/2020 katika ukumbi wa Ikulu Jijini
Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akihutubia baada ya kumaliza kuwaapisha Wakuu
wa Mikoa wa Zanzibar katika hafla iliofanyika ukumbi wa Ikulu Jijini
Zanzibar leo 3/12/2020.(Picha na Ikulu
WAKWANZA kutoka kushoto Spika wa Baraza la Wawakilishi
Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulid, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu
Mkuu Kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Mhe.Dkt. Mwinyi Talib Haji na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar
Kabi wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia baada
ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa wa Zanzibar aliowateua hivi karibuni, hafla
hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)WAKUU wa Mikoa Wapya wa Zanzibar wakifuatili kwa makini
hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.
Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) akihutubia baada ya kumaliza
kuwaapisha katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 3/12/2020.(Picha
na Ikulu)

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AZINDUA MAABARA MBILI

$
0
0
Katibu mkuu wa wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza katika hafla fupi ya kuzindua Maabara wilaya Arumeru mkoani Arusha.
Katibu mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Profesa Ole Gabriel wa Tatu Kushoto akiwa na Balozi wa Poland nchini Tanzania Mara baada ya kuzindua Maabara hizo.

Na.Mwandishi wetu Arusha.

Katibu mkuu wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Profesa Elisante Ole Gabriel amezindua maabara mbili ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA),Tengeru katika wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Akizungumza katika hafla fupi ya Uzunduzi wa maabara hizo Profesa Ole Gabriel alisema kuwa sekta ya Mifugo inathamani kubwa katika kuhakikisha kuwa inachangia Pato la Taifa kwa kiwango kikubwa,lakini bado haijafanya hivyo.

Ole Gabriel alisema kuwa vifaa hivyo ni muhimu kwa kuwa itawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo hali ambayo itaongeza uwezo katika masomo yao.

Aidha alisema kuwa Sayansi inahitajika katika kuhakikisha kuwa wafugaji wanabadili ufugaji na kuwa na Mifugo Bora zaidi pamoja na mazao yenye thamani ambayo yanatokana na Mifugo.

“Tunahitaji Sana Sayansi ya Mifugo ambayo itatusaidia kupata nyama bora,maziwa bora na hata bidhaa nyingine zote ili basi idadi tuliyonayo ya Mifugo iendane na thamani ya Mifugo yetu na hivyo tutapata Mifugo Bora zaidi”alisema Profesa Ole Gabriel

Hata hivyo alisema kuwa uwepo wa maabara hizo mbili pamoja na vifaa vitawezesha wanafunzi hao ambao wanakwenda kusaidia wafugaji wa chini katika kuhamilisha na kuchanja Mifugo kubobea katika sekta hiyo na Mifugo kuwa Bora zaidi.

Pia alisema kuwa mpango wa wizara hiyo bado ni kuboresha kosafu na mbari za mifugo,ili kupata Mifugo bora na bidhaa bora zaidi na hatimaye kuchangia Uchumi kwa asilimia 15 tofauti na Sasa Ambapo sekta hiyo inachangia 7.64.

Nae Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mifugo wa dkt.Pius Mwambene alisema kuwa vifaa hivyo vitawasaidia kuboresha mafunzo na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanawasaidia wafugaji katika kubadili ufugaji wa mazoea.

Alisema kuwa ni azma ya Serikali kuhakikisha kuwa inaboresha miundombinu Mbali Mbali ili kuhakikisha kuwa sekta ya mifugo inachangia ipasavyo pato la taifa.

Nchi ya Poland imekuwa ikiisaidia Serikali katika sekta ya Mifugo katika kuhakikisha kuwa inaongeza thamani ya mifugo ili kuongeza tija katika sekta hiyo.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA WAKANDARASI WANAWAKE NCHINI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Chama cha Wakandarasi Wanawake Nchini Bibi Judith Udunga aliyeongoza Ujumbe wa Wanachama wa Chama hicho walipomtembelea Makamu wa Rais katika Makazi yake Kilimani Jijini Dodoma leo Disemba 04,2020 kwa lengo la kuelezea changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

SERIKALI YAIMARISHA MIFUMO YA UKUSANYAJI WA MIRAHABA YA KAZI YA WASANII

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi namna serikali imeboresha kanuni za ukusanyaji wa mirabaha ya kazi za wasanii , leo Desemba 3, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika mkutano na Watayarishaji wa kazi za Muziki na Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s katika mkutano wa kujadli namna bora yakuisaiida sekta ya sanaa ili iweze kukua na kuendelea kufuatia ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ya kuendeleza sekta ya Sanaa.
Mtayarisha wa kazi za Filamu nchini William Mtitu akimuomba Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (hayupo pichani) kusaidia kupunguza utitiri wa kodi katika vifaa vya kuandalia filamu pamoja na makato ya kodi kwa kazi wanazozalisha, leo Desemba 03, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika mkutano na Watayarishaji wa kazi za Muziki na Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s, wa kujadili namna bora yakuisaiida sekta ya sanaa ili iweze kukua na kuendelea kufuatia ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ya kuendeleza sekta ya Sanaa.
Mwongozaji wa Sanaa za Maaonesho Bw. M Mwamnyenyerwa akiiomba serikali kujenga kumbi za kufanyia sanaa za maonesho katika kila mkoa ili kuendeleza sanaa hiyo inayoonekani kuanza kupotea nchini, leo Desemba 03, 2020, katika mkutano na Watayarishaji wa kazi za Muziki na Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s, wa kujadili namna bora yakuisaiida sekta ya sanaa ili iweze kukua na kuendelea kufuatia ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ya kuendeleza sekta ya Sanaa.
Baadhi ya Watayarishaji wa kazi za Muziki na Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi aliyeketi (watatu kushoto) leo Desemba 03, 2020 Jijini Dar es Salaam, mara baada ya kumaliza mkutano na Watayarishaji wa kazi za Muziki, Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s, wa kujadili namna bora yakuisaiida sekta ya sanaa ili iweze kukua na kuendelea kufuatia ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ya kuendeleza sekta ya Sanaa.
Dj Mkongwe Boniface Kilosa maarufu kama ‘DJ LOVE’ akiiomba serikali kuboresha mitaala ya elimu ya msingi katika masuala ya sanaa ili Sanaa iweze kuwa sehemu ya maisha ya watoto na kutambua vipaji vyao mapema, leo Desemba 03, 2020, katika mkutano na Watayarishaji wa kazi za Muziki na Filamu,Waongozaji wa Filamu na MaDJ’s, uliyofanyika Jijini Dar es Salaam kujadili namna bora yakusaidia sekta ya sanaa iweze kukua na kuendelea kufuatia ahadi ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ya kuendeleza sekta ya Sanaa.wa kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa Tanzania Bw.Godfrey Mngereza na wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Emmanuel Ishengoma.

Na Anitha Jonas – WHUSM, Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali amesema kuwa tangu COSOTA ihamie wizara hiyo imeboresha Kanuni mbalimbali ambazo zitasaidia kuongeza ukusanyaji wa mirabaha na imeongeza adhabu ya faini kutoka milioni 5 mpaka milioni 20 kwa mtu anayekamatwa na uharamia wa kazi za Sanaa, pia Kanuni hizo zimetoa nafasi ya Mtendaji wa COSOTA kuwa na mamlaka ya kutoza faini hiyo papo kwa papo.

Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo Desemba 03, 2020 Jijini Dar es Salaam katika mwendelezo wa mikutano yake ya kukutana na makundi mbalimbali ya Sanaa, ambapo kwa siku hii alikutana na MaDJ’s, Wataarishaji wa Muziki na Filamu na Waongozaji wa Filamu.

Akiendelea kuzungumza katika mkutano huo Dkt.Abbasi alitoa msisitizo kwa BASATA na Bodi ya Filamu kuweka juhudi zaidi katika kujenga sekta ya Sanaa badala ya kudhibiti au kufungia.

“Serikali kwa sasa ipo katika hatua za kuboresha mifumo ya hakimiliki ili kuhakikisha wasanii wa makundi yote wananufaika na ubunifu wa kazi zao kwa kila zinapotumika katika mazingira yoyote hivyo basi ni muhimu kwa kila msanii kusajili kazi yake ili aweze kunufaika na kwa upande wa waandaaji wa muziki ni vyema wakafahamu umuhimu wa kuwa na umiliki wa midundo ‘beats’ wanazoandaa na kusajili,”alisema Dkt. Abbasi.

Pamoja na hayo naye Mtendaji Mkuu wa COSOTA Doreen Sinare aliwasihi Watayarishaji wa kazi za Muziki kusajili kazi zao kwani hawawezi kupata haki zao kama hawatasajili ‘beats’ wanazoandaa, ambapo alifafanua mara nyingi imekuwa ikionekana kama Mwanamuziki ndiyo mwenye umiliki wa kila kitu katika muziki na ubunifu wa mtayarishai huyo kusahaulika.

Halikadhalika katika mkutano huo Dkt. Abbasi aliwasihi wadau wa Sanaa kuanisha utitiri wa kodi zinazosumbua sekta hiyo ili serikalini iweza kujenga hoja ya namna zinaweza kupunguzwa,pia aliwasihi wasanii hao kuanisha mahitaji ya mafunzo yatakayowasaidia kuongeza ufanisi katika kutekeleza kazi zao kwa kushirikiana na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)

WAHITIMU VETA WATAKIWA KUJIJENGEA UTAMADUNI WA KUJIAJIRI KULIKO KUSUBIRI KUAJIRIWA

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Mhe.Deogratius Lukomanya(mgeni rasmi) akizungumza katika mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya Ufundi Stadi na huduma daraja la pili (NVA Level !!) na la tatu (NVA Level !!!)VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo VETA Chang’ombe Bw.Joseph Mwanda akizungumza mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya Ufundi Stadi na huduma daraja la pili (NVA Level !!) na la tatu (NVA Level !!!)VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanamitindo wakionesha mavazi ambayo yamebuniwa na wanafunzi wa chuo cha VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam katika mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya Ufundi Stadi na huduma daraja la pili (NVA Level !!) na la tatu (NVA Level !!!)VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam
Wanafunzi wa Chuo cha VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam wakiimba na wakicheza muziki (bendi) katika mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya Ufundi Stadi na huduma daraja la pili (NVA Level !!) na la tatu (NVA Level !!!)VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Wahitimu wa Chuo Cha Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA wametakiwa kuwa na moyo wa kufanya kazi kwa kujituma hasa kwa ujuzi walioupata Chuoni ili waweze kupata mafanikio.

Akizungumza katika mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya Ufundi Stadi na huduma daraja la pili (NVA Level !!) na la tatu (NVA Level !!!)VETA Chang’ombe Jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Mhe.Deogratius Lukomanya amewataka waondokane na dhana ya kuletewa ajira bali wajitume kwa kujitengenezea ajira.

“Katika karne hii ya 21 upatikanaji wa ajira umekuwa ni changamoto kubwa ulimwenguni kote, ni wajibu wenu kuwa na mawazo ya kujitengenezea ajira zenu wenyewe kwa ujuzi mliopata”. Amesema Mhe.Lukomanya.

Aidha Mhe.Lukomanya amewataka wahitimu waendelee kuwa waminifu na moyo wa kufanya kazi kwa kujituma katika sehemu zao za kazi ili waweze kupata mafanikio.

Hata hivyo, amewaomba waajiri kuendelea kupokea vijana na kuwapatia nafasi za mafunzo kwa vitendo viwandani pamoja na nafasi za ajira kwa vijana pale zitakapopatikana.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo VETA Chang’ombe Bw.Joseph Mwanda amesema kuwa mwaka huu 2020 Chuo kimeweza kusajili jumla ya wanafunzi 1,361 wa mwaka wa kwanza, wa pili na wa tatu kwa kozi za muda mrefu na diploma ya ubunifu wa mitindo ya mavazi.

Amesema Chuo hicho kina wanafunzi wenye mahitaji maalumu ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu wa mfumo wa fahamu na watu wenye ulemavu wa viungo ambapo wengi wao wameonyesha uwezo mkubwa kwenye mafunzo yao.

” Kwa mwaka huu 2020 tuna wanafunzi wenye mahitaji maalumu 21 katika fani mbalimbali. Kati yao wanafunzi 10 ni wenye ulemavu wa mfumo wa akili na wanafunzi 11 ni wenye ulemavu wa viungo”. Amesema Bw.Mwanda.

Hata hivyo Bw.Mwenda amesema changamoto kubwa ambazo wanakumbana nazo ni pamoja na uhaba wa majengo na samani kwaajili ya wanafunzi wa kozi ndefu na fupi kwa karibu nusu ya mahitaji.

Akizungumza kwa niaba ya wazazi wote Bi.Avelina Mrema amewahimiza wahitimu kutokata tamaa katika maisha yao kwani ndio ukurasa mpya umefunguliwa

Magufuli Ateua Baraza la Mawaziri

$
0
0
RAIS John Magufuli, leo Desemba 5, 2020, ameteua baraza la mawaziri ambapo orodha hiyo imesomwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ni Elias Kwandikwa, Wizara Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ni Capt. Mst. George Mkuchika.

Wizara ya Ardhi ni William Lukuvi, Wizara ya Maji ni Juma Aweso, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ni Innocent Bashungwa, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ni Jenista Mhagama

Wizara ya Afya ni Dkt. Dorothy Gwajima, ambaye pia rais amemtea kuwa Mbunge, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uwekezaji ni Prof. Kitila Mkumbo, Wizara ya Katiba na Sheria -ni. Dkt. Mwigulu Nchemba naWizara ya Elimu -niProf. Joyce Ndalichako.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni Mashimba Mashauri Ndaki, Wizara ya Maliasili na Utalii ni Dkt. Ndumbaro Damas Daniel, Ofisi ya Rais TAMISEMI ni. Selemani Jafo, Wizara ya Nishati ni Dkt. Medard Kalemani, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ni Leonard Chamuriho na Wizara ya Kilimo ni Prof. Adolf Mkenda.

Wizara ya Madini ni Dkt. Doto Biteko, Wizara ya Viwanda na Biashara ni Geoffrey Mwambe, na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ni George Simbachawene

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira ni Ummy Mwalimu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (wizara mpya) ni Dkt. Faustine Ndugulile

KILIMO CHA BUSTANI KIMEAJIRI WATU MILIONI NNE-MAJALIWA

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungunza kwenye mkutano wa kanda wa uwekezaji katika sekta ya Mazao ya Bustani (Horticulture) uliyofanyika Disemba 5, 2020 kwenye Hoteli ya Hyat Regency, Jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongea na Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya Wazalishaji wa Mbogamboga na Matunda Tanzania (TAHA) Mhandisi Zebadiya Moshi, wakati wa mkutano wa kanda wa uwekezaji katika sekta ya Mazao ya Bustani (Horticulture) uliyofanyika Disemba 5, 2020 kwenye Hoteli ya Hyat Regency, Jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Abubakar Kunenge, Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya Wazalishaji wa Mbogamboga na Matunda Tanzania (TAHA) Mhandisi Zebadiya Moshi na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya. Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya akiongea na wadau wa sekta ya mazao ya bustani (Horticulture) wakati wa mkutano wa kanda wa uwekezaji katika sekta hiyo Disemba 5, 2020 Jijini Dar es salaam, kwenye Hoteli ya Hyat Regency, Jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya Wazalishaji wa Mbogamboga na Matunda Tanzania (TAHA) Mhandisi Zebadiya Moshi akimkabidhi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa taarifa ya changamoto zilizopo katika kilimo cha Mbogamboga, Disemba 5, 2020 Jijini Dar es salaam, kwenye Hoteli ya Hyat Regency, Jijini Dar es salaam.

*Aiagiza Wizara ya Kilimo ianzishe kituo cha utafiti wa mazao hayo

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema tasnia ya kilimo cha mazao ya bustani ina mchango mkubwa kwenye maendeleo ya uchumi nchini na kuajiri watu zaidi ya milioni nne, hivyo kuongeza kipato kwa wakulima na wafanyabiashara wengi.

Kufuatia umuhimu wa tasnia hiyo katika ukuaji wa uchumi wa Taifa, Waziri Mkuu ameaiagiza Wizara ya kilimo ianzishe Mamlaka ya Horticulture na Kituo cha Utafiti kwa ajili ya kusimamia na kuratibu mazao ya matunda, viungo na mbogamboga tu.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Desemba 5, 2020) baada ya kufungua Kongamano la Kikanda la Biashara la Uwekezaji katika Tasnia ya Mazao ya Bustani lililofanyika kwenye Hoteli ya The Kilimanjaro Hyatt Regency, jijiji Dar es Salaam.

“Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita uzalishaji wa mazao ya bustani nchini uliongezeka kwa asilimia 10.5 kutoka tani 5,931,900 mwaka 2015/2016 hadi kufikia tani 6,556,102 mwaka 2018/2019.”

Amesema takwimu hizo zinathibitisha ukuaji wa tasnia hiyo na uwepo wa haja ya kuweka mikakati ya kuiendeleza zaidi. “Hivyo basi, kwa kuwa bei kwa tani inakadiriwa kuwa shilingi 500,000 thamani ya mazao ya kilimo cha mazao ya bustani kwa mwaka 2018/2019 inakadiriwa kuwa kiasi cha shilingi trilioni 3.3.”

Waziri Mkuu amesema mbali na kuchangia katika ukuaji wa uchumi, tasnia hiyo inasaidia kujenga Taifa lenye watu wenye afya nzuri, nguvu na uwezo wa kufanya kazi, pia ni chanzo kikuu cha lishe na afya bora kwa Watanzania kutokana na virutubisho vingi kwa ulaji wa mbogamboga, matunda na viungo.

Amesema mazao ya bustani yamekuwa na mchango mkubwa katika kupambana na gonjwa hatari la Covid-19 kwa sababu dawa mbadala za asili zilizosaidia wananchi wengi duniani kote kudhibiti ugonjwa huo zilitokana na matunda na viungo.

“Kutokana na vilelezo hivyo, ni wazi kuwa mchango wa tasnia ya kilimo cha mazao ya bustani kwenye maendeleo ya watu na uchumi wa nchi yetu na dunia kwa ujumla ni mkubwa na iwapo fursa zilizopo zitafanyiwa kazi, basi safari yetu ya kuelekea kwenye uchumi ulio imara zaidi itakuwa ya mafanikio makubwa, kwa kipindi kifupi.”

Wakati Huo huo, Waziri Mkuu amesema katika kuimarisha miundombinu ya usafirishaji ili kuwezesha biashara hususan ya mazao yanayoharibika haraka kama mazao ya bustani, minofu ya samaki na nyama, Serikali kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020 – 2025, imepanga kununua ndege ya mizigo kwa kuzingatia mahitaji ya biashara na ukuaji wa uchumi.

“Pamoja na ndege ya mizigo tutanunua ndege kubwa mbili za masafa marefu na ndege mbili za masafa ya kati ili kuongeza fursa za biashara. Pia Serikali imeunda kamati maalum inayojumuisha wataalamu wa Serikali na wale wa sekta binafsi, ambayo imeanza kuainisha changamoto za usafirishaji na za kimfumo katika bandari na viwanja vyetu vya ndege ili kufanya maboresho yanayohitajika na hivyo tuweze kutumia miundombinu ya ndani katika kusafirisha bidhaa zetu.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuziagiza taasisi zote zinazohusika na usafirishaji wa mizigo kwa njia ya anga na bahari pamoja na kamati iliyoundwa kusimamia zoezi hilo zifanyie kazi kwa haraka mapendekezo ya wataalamu yatakayotokana na utafiti unaoendelea kuhusu kuboresha miundombinu na mifumo ya usafirishaji.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya alisema kutokana na umuhimu wa tasnia hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa zao hilo wameendelea kufanya uchambuzi wa athari za wadudu kwa ajili ya baadhi ya masoko mapya kama China, India na Afrika Kusini.

Pia, Bw. Kusaya alisema kutokana na umuhimu wa tasnia hiyo Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo ili iendelee kutoa mchango mkubwa katika Taifa na hivyo kuwezesha ukuaji wa uchumi, ajira na upatikanaji wa malighafi za viwandani

NAIBU KATIBU MKUU,WIZARA YA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO AWAFUNDA VIJANA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

$
0
0

Jane Edward fullshangweblog,Arusha

Naibu Katibu mkuu wizara ya Ujenzi uchukuzi na mawasiliano Sekta ya mawasiliano Dkt. Jim Yonazi amesema ni vema wabunifu waliopo katika jamii wakatambuliwa bila kuangalia kuwa ni wanafunzi katika vyuo mbalimbali ili waweze kuendelezwa katika ubunifu wao.

Dkt Yonaz ameyasema hayo wakati akifungua kongamano la ubunifu kwa vijana mkoani Arusha lililofanyika katika Chuo cha Uhasibu Kilichopo Njiro mkoani hapa.

Aidha Dkt. Yonaz alisema wapo wabunifu wengi katika jamii lakini hawatambuliwi kutokana na kwamba siyo wanafunzi wa vyuo hivyo kazi zao hazijatambuliwa.

“Wabunifu ambao hawapo vyuoni watambuliwe ili waweze kuendelezwa msiishie hapa tu chuoni hapana, jamii inawatu wanaobuni vitu mbalimbali lakini hawajaletwa pamoja kama ambavyo mnakusanya vijana kutoka vyuo mbalimbali kuonyesha ubunifu wao” alisema.

Alitoa pia maagizo kwa wanatehama kujisajili katika tume ya Tehama lengo likiwa kupata haki zao za Msingi kupitia Tume ambapo alivitaka vyuo vilivyoanzisha vituo vya kuleta vijana pamoja kuhakiki kila baada ya makongamano wanayoandaa wanapeleka majina katika tume hiyo ili washiriki wa kongamano waweze kutambuliwa.

Naye mkuu wa chuo cha Uhasibu Arusha Prof. Eliamani Sedoyeka alisema kutokana na uhitaji wa vijana kuwa mkubwa wa kutaka kuonyesha bunifu zao waliona waanzishe kituo cha uvumbuzi (Innovation Summit)kwa ajili ya makongamano ya vijana kuonyesha ubunifu mbalimbali.

“Tumefanikiwa kutoa vijana 100 wanaoweza kujitegemea kwa kuweza kusimamia Kazi zao za ujasiriamali bila kusubiri ajira peke yake, na tunashukuru Ofisi ya mkurugenzi Arusha imetupa ushirikiano kwa kiasi kikubwa kwani Mkurugenzi ameahidi kutoa sapoti kwa makundi yaliyokidhi vigezo katika zile asilimia tano za vijana zinazotolewa na jiji” alisema Prof Sedoyeka.

Naye mkurugenzi wa jiji hilo Dkt John Pima alisema watatoa ushirikiano 100% kwa vikundi vitakavyo kidhi vigezo vya kupewa mikopo hiyo kama kutambua mchango wa vijana katika serikali ya awamu ya tano.

Kwa upande wake msimamizi wa Kongamano hilo bi Pamela Choga alisema mashindano ya ubunifu yalifunguliwa rasmi nov 23 mwaka huu na yaliruhusu kila kijana kuonyesha kazi zake za ubunifu ambapo hatua ya kwanza washiriki walitakiwa kuonyesha video fupi inayoonyesha kazi alizobuni, na hatua ya mwisho ni kushiriki kwa njia ya kuonyesha bidhaa mbalimbali zilizobuniwa na baadaye washindi walipatiwa zawadi.

Mshindi wa kwanza hadi wa tatu kila kundi alipatiwa zawadi na cheti cha ushiriki ambapo mshindi wa kwanza alipatiwa fedha taslimu sh. 500,000 , mshindi wa pili sh. Laki tatu na wa tatu sh. Laki mbili.

Tanzania yafungua ofisi ya Mwakilishi wa Heshima jijini Mumbai

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda kwa pamoja na Mwakilishi wa Heshima Mteule wa Tanzania jijini Mumbai Bwana Nayan Patel wakisaini Mkataba wa Kazi wa kumwezesha Bwana Patel kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania katika mji huo. Mkataba huo ulisainiwa jijini Mumbai, India tarehe 04 Desemba 2020.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda na Bwana Nayan Patel wakibadilishana Mkataba wa Kazi wa kumwezesha Bwana Patel kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania katika mji wa Mumbai.
Mwakilishi
wa Heshima wa Tanzania Jijini Mumbai Bwana Nayan Patel akihutubia
katika hafla ya ufunguzi rasmi wa ofisi ya
Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania Jijini humo iliyofanyika tarehe 04 Desemba
2020.
Balozi wa Tanzania
nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akitoa hotuba kumpongeza Bwana Patel kwa
kukubali kuiwakilisha Tanzania jijini Mumbai na kumtaka kuiwakilisha vema nchi.
Balozi wa Tamzania nchini
India, Mhe. Baraka Luvanda na Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania Jijini Mumbai
Bwana Nayan Patel wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni walioshriki
halfla ya uwekaji saini wa Mkataba wa Kazi wa Mwakilishi wa Heshima.

Na. Mwandishi Maalum, India

Tanzania yafungua ofisi ya Mwakilishi
wa Heshima jijini Mumbai

Serikali ya Tanzania imefungua rasmi
ofisi ya Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania katika Jiji la Mumbai katika hafla
iliyofanyika jijini humo tarehe 04 Desemba 2020.

Mumbai ni jiji kuu la biashara na
viwanda nchini India (commercial and industrial hub) ambapo linachangia zaidi
ya asilimia 6 la pato la India na pia linachangia zaidi ya asilimia 25 ya
uzalishaji wa bidhaa mbalimbali za viwandani nchini India (25% of industrial
output).

Aidha, Mumbai ni jiji mojawapo kati
ya majiji kumi duniani, yanayoongoza kwa biashara, hususan katika mzunguko wa
fedha duniani (global financial flow). Vilevile, Mumbai ni Jiji linaloongoza
kuwa na mabilionea wengi nchini India, ambapo linashika nafasi ya 9 kuwa na
mabilionea wengi duniani.

Kadhalika, shughuli za biashara na
huduma za kifedha katika Jiji hilo lenye watu zaidi ya milioni 20 zinachangia
mzunguko wa fedha katika uchumi wa India kwa zaidi ya asilimia 70.

Ni kutokana na umuhimu wa Jiji hilo,
Serikali iliamua kusogeza karibu huduma za kikonseli, biashara, uwekezaji,
utalii na mengineyo kwa kuwa na Mwakilishi wa Heshima atakayeratibu shughuli
hizo kwa karibu. Ikumbukwe India ni nchi kubwa yenye uchumi mkubwa na idadi
kubwa ya watu duniani wanaofikia bilioni 1.2. Hivyo, si rahisi kwa nchi zenye
uwakilishi mjini New Delhi kuweza kuhudumia kwa ukamilifu nchini India bila
kuwa na ofisi za aina hii.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Balozi
wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda alielezea juu ya umuhimu wa ofisi
ya Mwakilishi wa Heshima jijini Mumbai kuwa itasaidia kutoa huduma za Kikonseli
kwa karibu zaidi na pia itasaidia zaidi kuvutia na kutangaza fursa mbalimbali
za biashara, uwekezaji zilizopo nchini, kutafuta masoko ya bidhaa za kilimo na
viwanda vya Tanzania pamoja na vivutio mbalimbali vya utalii wa Tanzania ili
kukuza sekta ya utalii nchini.

Aidha, Balozi Luvanda alieleza kuwa
ofisi hiyo itachangia katika kukuza biashara zaidi kati ya Jiji la Dar es
Salaam na Mumbai kufuatia kuimarishwa kwa huduma za usafiri wa anga baada ya
Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania) kuanza safari zake za ndege za moja
kwa moja kutoka Dar es Salaam kwenda Mumbai tangu mwezi Julai 2019. Vilevile,
majiji haya yanaunganishwa na bandari kuu muhimu ambazo ni Bandari ya Dar es
Salaam, kwa upande wa Tanzania, na Bandari ya Mumbai, kwa upande wa India.

Bwana Nayan Patel, ni raia wa India
na mfanyabiashara mwenye mtaji mkubwa jijini Mumbai na amekwishaanza rasmi kazi
ya Uwakilishi wa Heshima baada ya kukamilika kwa taratibu zote za
kidiplomasia.

Bwana Patel aliishukuru Serikali ya
Tanzania kwa kumpa heshima kubwa ya kuiwakilisha Tanzania jijini Mumbai na
maeneo mengine ya jirani na akaahidi kuitendea haki nafasi hiyo kadri
atakavyoweza.

WAZIRI WA KILIMO-ZANZIBAR MHE. DKT. SOUD HASSAN AFUNGUA KONGAMANO LA WENYE-VIWANDA NA TAASISI ZA UTHIBIT

$
0
0
Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji na Mifugo wa Zanzibar Mhe. Soud Hassan akifungua kongamano la biashara kati ya Taasisi za Serikali pamoja na wamiliki wa viwanda nchini leo, 05 Desemba 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere – Dar es Salaam ambalo limelenga kutatua changamoto zinazowakabili wamiliki wa viwanda katika uendeshaji wa shughuli za uzalishaji wa bidhaa nchini katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 hadi 9 Desemba, 2020. Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe akitoa maelezo ya utangulizi wakati wa ufunguzi wa kongamano la biashara kati ya taasisi za Serikali pamoja na wamiliki wa viwanda nchini, Leo 05 Desemba 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere – Dar es Salaam ambalo limelenga kutatua changamoto zinazowakabili wamiliki wa viwanda katika uendeshaji wa shughuli za uzalishaji wa bidhaa nchini katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 hadi 9 Desemba, 2020.Baadhi ya wadauwa sekta ya Viwanda nchini na washiriki wa kongamano la biashara kati ya taasisi za Serikali pamoja na wamiliki wa viwanda nchini, leo 05 Desemba 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere – Dar es Salaam ambalo limelenga kutatua changamoto zinazowakabili wamiliki wa viwanda katika uendeshaji wa shughuli za uzalishaji wa bidhaa nchini katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 hadi 9 Desemba, 2020..Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji na Mifugo wa Zanzibar Mhe. Soud Hassan (aliyekaa wa pili kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. ,Riziki Shemdoe (aliyekaa wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Taasisi ya TanTrade, Ndg. Edwin Rutageruka wakiwa katika picha na wadau wa sekta ya viwanda nchini na wamiliki wa viwanda nchini waliohudhulia katika kongamano la biashara kati ya Taasisi za Serikali pamoja na wamiliki wa viwanda nchini, Leo 05 Desemba 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere – Dar es Salaam katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 hadi 9 Desemba, 2020.

Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji na Mifugo wa Zanzibar Mhe. Soud Hassan (aliyekaa wa pili kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. ,Riziki Shemdoe (aliyekaa wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Taasisi ya TanTrade, Ndg. Edwin Rutageruka wakiwa katika picha na wakurugezi wa Taasisi za Serikali waliohudhulia katika kongamano la biashara kati ya Taasisi za Serikali pamoja na wamiliki wa viwanda nchini, Leo 05 Desemba 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere – Dar es Salaam katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania yaliyoanza tarehe 3 hadi 9 Desemba, 2020. (Picha na Eliud Rwechungura)

Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara hatua inayoongeza kasi ya uwekezaji hasa katika viwanda na biashara, na tayari tumeanza mafanikio yameanza kuonekana.

Ameyasema hayo leo Waziri Wa Kilimo, Umwagiliaji, Mali Asili Na Mifugo – Serikali Ya Mapinduzi – Zanzibar Mhe. Dkt. Soud Nahoda Hassan akifungua Kongamano La Wenye-Viwanda Na Taasisi Za Uthibiti katika Maonesho ya Tano ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Maonesho wa Julius Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam.

“Serikali imefanikiwa kuandaa na kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Udhibiti wa Biashara Nchini – BLUEPRINT. Mpango huo umewezesha maboresho ya tozo, ada na adhabu. jumla ya tozo, ada na adhabu mia mbili thelathini na mbili (232) zimefutwa au kupunguzwa na Serikali”. Amesema Mhe.Dkt.Hassan.

Aidha Mhe.Dkt.Hassan amesema hatua ambayo imefikiwa miaka mitano kabla ilivyokuwa imetarajiwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025. Serikali imefanikiwa kuwavutia wawekezaji makini na mahiri kutoka hapa nchini na nje ya nchi kuja kuwekeza katika viwanda vidogo, vya kati na vikubwa.

Hata hivyo amesema Sekta hiyo imeendelea kuchangia katika Pato la Taifa kwa mfano mwaka 2019 ilichangia kwa asilimia 8.5 ikilinganishwa na asilimia 8.05 mwaka 2018, sawa na ongezeko la asilimia 0.45.

“Kasi ya ukuaji wa thamani ya Uzalishaji Bidhaa Viwandani kwa mwaka 2019 ilikuwa ni Shilingi Trilioni 10.2 ikilinganishwa na Shilingi Trilioni 9.6 mwaka 2018, sawa na kasi ya ukuaji wa asilimia 5.8”. Ameeleza Mhe.Dkt.Hassan.

Nae Mkurugenzi Mkuu Wa Mamlaka Ya Maendeleo Ya Biashara Tanzania (Tantrade), Bw. Edwin N. Rutageruka amesema TanTrade imekuwa ikiratibu Kliniki ya Biashara (Business Clinic) kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali kutoka Taasisi za Uthibiti ili kutatua kero zinazokwaza uzalishaji katika sekta ya viwanda na biashara.

Vilevile amesema Mikutano hiyo inatoa fursa ya kuwakutanisha wanunuzi na wauzaji kujadili na kutathmini kiasi na ubora wa upatikanaji wa bidhaa, malighafi, aina, mashine, teknolojia, kuhifadhi, kusindika na kufungasha kwa kupanga mkakati wa suluhu ya changamoto na kuanzisha mahusiano endelevu ya biashara.

“Mikutano hii imelenga kuhamasisha ustawi wa viwanda hapa nchini kupitia uongezaji thamani mazao yanayozalishwa nchini na bidhaa zake ili kupata masoko endelevu ya ndani, kikanda na kimataifa”. Amesema Bw.Rutageruka.

CSI WAENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU AFYA YA MAMA NA MTOTO ILI KUPUNGUZA VIFO VINAVYOTOKEA WAKATI WA KUJIFUNGUA

$
0
0

 Meneja wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival International(CSI) Ester Mpanda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna walivyohamasika kudhamini  pamoja na kutoa elimu kuhusu makuzi ya mtoto hasa katika kudhibiti vifo vitokanavyo na uzazi kwa mama na mtoto wakati wa kujifungua na vifo wakati wa tukio la kukabidhiwa fedha kwa Shule ya Msingi Sinza Maalum ambazo zinakwenda kufanikisha ujenzi wa vyoo na bafu kwenye shule hiyo ambayo kuna wanafunzi wenye mahitaji maalum ziilizochangishwa na Kampuni ya Open_ Kitchen .

Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kijitonyama Dama Lusangija(kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival International(CSI) Ester Mpanda kuhusu kazi zinazofanywa na Shirika hilo hasa hasa katika kudhibiti vifo vitokanavyo na uzazi kwa mama na mtoto wakati wa kujifungua na vifo cha watoto wenye umri chini ya miaka mitano wakati wa tukio la kukabidhiwa fedha kwa Shule ya Msingi Sinza Maalum ambazo zinakwenda kufanikisha ujenzi wa vyoo na bafu kwenye shule hiyo ambayo kuna wanafunzi wenye mahitaji maalum ziilizochangishwa na Kampuni ya Open_ Kitchen.

Meneja wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival International(CSI) Ester Mpanda akitoa elimu kwa baadhi ya wanawake  waliofika kwenye hafla ya kukabidhiwa fedha kwa Shule ya Msingi Sinza  Maalum ambazo zinakwenda kufanikisha ujenzi wa vyoo na bafu kwenye shule hiyo ambayo kuna wanafunzi wenye mahitaji maalum ziilizochangishwa na Kampuni ya Open_ Kitchen.Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kijitonyama Dama Lusangija akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya kijamii mara baada ya kukabidhi fedha kwa Shule ya Msingi Sinza Maalum.Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kijitonyama Dama Lusangija  akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa shirika la Childbirth Survival International(CSI)  pamoja na uongozi wa Kampuni ya Open_ Kitchen.


SHIRIKA la Childbirth Survival International(CSI) ambalo linajihusisha na afya ya Mama na Mtoto hasa katika kudhibiti vifo vitokanavyo na uzazi kwa mama na mtoto wakati wa kujifungua na vifo cha watoto wenye umri chini ya miaka mitano limesema litaendelea kuzungumzia umuhimu wa jamii kushiriki kikamilifu kupunguza vifo vinavyotokea wakati wa kujifunga.

CSI limesema hayo leo Desemba 6, 2020 jijini Dar es Salaam wakati wa tukio la kukabidhiwa fedha kwa Shule ya Msingi Sinza Maalum ambazo zitakwenda kufanikisha ujenzi wa vyoo na bafu kwenye shule hiyo ambayo kuna wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Hivyo pamoja na wadau wengine wa maendeleo kushiriki katika tukio hilo CSI kutokana na umuhimu wao kwenye jamii nayo ilipewa nafasi ya kushiriki na kutoa elimu ya afya ya uzazi ambayo itasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Uchangishaji wa fedha hizo kiasi cha Sh.milioni 11 umefanywa na Amka Twende Golden Women ambayo ipo chini ya Kampuni ya Open_Kitchen ambayo imejikita kuwawezesha na kuwasaidia wanawake wajasiriamali chini ya Mkurugenzi wake Upendo Mwalongo kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo.

Akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo maofisa kutoka serikalini, wadau wa maendeleo , wanawake wajasiriamali , Mwakilishi kutoka CSI ambaye ni Meneja wa Programu za Vijana katika shirika hilo Ester Mpanda amefafanua wanajihusisha na afya ya mama na mtoto na lengo ni kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifunga na wale wenye umri chini ya miaka mitano.

Amesema CSI makao makuu yake yapo nchini Marekani lakini wanayo ofisi yao nchini Tanzania pamoja na matawi mengine kaika nchi za Rwanda na Kenya na lengo kuu ni kuhakikisha vifo vya mama na mtoto vinapungua au kwisha kabisa.

"CSI mbali ya kuwa Marekani iko pia Tanzania, ni shirika la kimataifa ambalo limeanzishwa na wamama wawili ambao ni Tausi Swed Kagasheki ambaye anaishi Marekani na mama Stella Mpanda ambaye yuko nchini Tanzania.

"Tuko hapa kwenye Amka Twende kwasababu tunaona ni nafasi kwetu sisi kuzungumzia masuala yanayohusu afya ya mama na mtoto ambayo tunaamini inawahusu na akina , suala la afya ya mama na mtoto sio la mama peke yake bali na baba naye anahusika maana sote tunahusika katika kuhakikisha maisha ya mama na mtoto yanakuwa salama,"amesema Ester Mpanda.

Ameongeza hivyo wanamshukuru Upendo Mwalongo kwa kuwapa nafasi hiyo ya kuungana na Kampuni ya Open_ Kitchen inayosimamia mradi wa Amka Twende na timu yake ili kuzungumzia kwa kina kuhusu shirika hilo na majukumu yake.Pia amesema CSI inapongeza na kuishukuru Serikali kwa jitihada zake za kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo shirika hilo la kimataifa.

Ester Mpanda kupitia meza yao ya kutoa elimu iliyokuwepo kwenye eneo hilo, ilikuwa na jukumu la kuhakikisha elimu kuhusu usalama wa afya ya mama na mtoto inawafikia wageni waliokuwa wamehudhuria na miongoni mwa waliopata nafasi ya kufika kwenye meza ya CSI ni mgeni rasmi ambaye ni Diwani wa Kata ya Kijitonyama Dama Lusangija.

Kwa upande wake Upendo Mwalongo alipata nafasi ya kumtambulisha Ester Mpanda kwa wadau mbalimbali wa maendeleo waliohudhuria tukio hilo la ukabidhiwaji fedha huku akionesha kufurahishwa na kile ambacho CSI wanafanya katika jamii kuhakiksha vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua na vile vya watoto chini ya miaka mitano vinakwisha.

VIVUTIO VYA TANZANIA KUTANGAZWA KWENYE TELEVISHENI YA UFARANSA

$
0
0
Mkuu wa Ofisi ya TTB Kanda ya Kaskazini Bi. Esta Solomoni akiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro pamoja na Sebastian Verlet (katikati) na Maxime Souville Wataalam kutoka Bo Travail ya Ufaransa

Wataalam kutoka Bo Travail ya Ufaransa, Sebastian Verlet (kushoto) na Maxime Souville wakionyesha mifuko waliyokabidhiwa na TTB yenye vipeperushi vyenye taarifa za vivutio vya utalii vya Tanzania.

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa imeandaa ziara ya Wataalmu nane watengeneza filamu za utalii kutoka katika kampuni ya Bo Travail ya nchini Ufaransa kwa lengo la kutengeneza filamu ya kitalii iliyopewa jina la “Tanzania Beautiful Escapes” pamoja na makala maalumu ya lugha ya kifarasa ambazo zitaonyeshwa kwenye Televisheni ya Ufaransa.

Akizungumza punde baada ya kundi la kwanza la wataalam wawili wa Bo Travail kuwasili katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Kilimanjaro tarehe 5 Disemba, 2020, Mratibu wa safari hiyo ambaye ni Mkuu wa ofisi ya TTB Kanda ya Ziwa, Bi. Glory Munhambo alisema “TTB imefaya jitihada za makusudi kushirikiana na kampuni ya Bo Travail ambayo ni watengeneza filamu mashuhuri za utalii nchini Ufaransa kuja Tanzania kutayarisha filamu na makala kwa kutumia baadhi ya maeneo ya vivutio vya utalii vya jiji la Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha, Karatu kwenye vikundi vya utalii wa kiutamaduni na visiwa vya Zanzibar .

Bi. Glory aliendelea kusema kuwa “Wataalamu hawa watakuwa nchini kwa muda wa siku 14, ambapo wanawasili kwa makundi mawili tofauti, kundi la kwanza la watu wawili limeingia leo na kuondoka Disemba 18, 2020 na kundi la pili la wataalamu wanne litawasili nchini Disemba 8 mpaka Disemba 18, 2020, huu ni mwendelezo wa mpango mkakati wa TTB wa kutumia vipindi maalumu vya televisheni za nchi mbalimbali ili kuweza kufikisha ujumbe kwa watu wengi zaidi katika masoko ya utalii na kuwavitia ili waje kuvitembelea vivutio vya utalii vya Tanzania.”

Ufaransa ni moja ya masoko makuu ya utalii ya Tanzania barani ulaya ambapo kwa takwimu za mwaka 2019 zinazotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii zinaonyesha Tanzania ilipokea jumla ya watalii 56, 297 kutoka Ufaransa.


TANZANIA YAUNGA MKONO AZIMIO LA AU KUONGEZA MIAKA 10 YA KUONDOA NA KUTOKOMEZA SILAHA HARAMU

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi akichangia moja ya agenda katika mkutano wa 14 wa dharua Umoja wa Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference) jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi akiwa pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe pamoja na washiriki wengine wakifuatilia mkutano wa 14 wa dharua Umoja wa Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference)

Umoja wa Afrika (AU) umezitaka nchi wanachama wa umoja huo kutilia mkazo azimio la kuondoa na kutokomeza silaha haramu ili kuliondoka na migogoro inayolifanya bara hilo kushindwa kusonga mbele kiuchumi.

Akifungua Mkutano wa 14 wa dharura wa Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference) Mwenyekiti wa Umoja huo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa amesema ni vigumu Bara la Afrika kupiga hatua za kimaendeleo kiuchumi endapo suala la usalama halitapewa kipaumbele na kuruhusu migogoro kuendelea.

Rais, Ramaphosa ameongeza kuwa wakati umefika kwa nchi za afrika hususani zilizopo katika migogoro na vita kuhakikisha kuwa zinatatua vyanzo vya machafuko hayo na kuboresha hali ya kiuchumi kwa wananchi, utawala wa sheria, na kuzingatia misingi ya haki na utawala bora.

Akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Meh. John Pombe Joseph Magufuli katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi amesema mkutano huo ulikuwa unajadili mpango na mkakati wa miaka 10 iliyopita wa kuondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika.

“Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeunga mkono azimio la nchi za AU kuongeza miaka mingine 10 ya kutokomeza silaha haramu na kusisitiza tena ushiriki wake kikamilifu katika kuhakikisha kuwa Afrika inatatua migogoro yake yote yenyewe bila kuingiliwa na nchi za nje, lakini pia kuzitaka nchi za Afrika kuzuia mitafaruku na migogoro yote ambayo kwa miaka mingi imeigharimu sana bara la Afrika,” Amesema Prof. Kabudi

Prof. Kabudi ameongeza kuwa, toka hatua ya kuondoa na kutokomeza silaha haramu ilipoanza mwaka 2017 hadi 2019, silaha zaidi ya 1,233 zimerejeshwa na Serikali itaendelea na jitihada ya kuhakikisha kuwa inazitambua silaha zote.

Aidha, Prof. Kabudi ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi zote ili kuwa na amani endelevu na utulivu endelevu katika eneo lote la Maziwa Makuu, pia Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa mchango wake katika nchi mbalimbali zenye mapigano ikiwemo DRC halikadhalika katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na sehemu nyingine ambapo vikosi vyake vya kijeshi vitatumwa kulinda amani.

Nae Rais wa Ghana, Mhe. Nana Akufo-Addo amesema kuwa Ghana inaungana na Umoja wa Afrika (AU) na itaendelea kuhakikisha inaondoa na kutokomeza silaha haramu kwa lengo la kuimarisha masuala ya Amani, umoja na ushirikiano wa nchi za AU.

“Ghana tangu mwaka 2014 tulishaanza mkakati wa kuzuia na kutokomeza matumizi holela silaha haramu kwa kuzihakiki na kuandikisha wamiliki wote wanaomiliki silaha,….….pia mwaka jana 2019 kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) tumeweza kuendelea kudhibiti silaha matumizi ya silaha holela,” Amesema Rais Akufo-Addo

Nae Rais wa Somalia, Mhe. Mohamed Farmajo amesema kuwa suala la Amani na usalama ni suala muhimu sana kwenye jamii hivyo Somalia inaungana na Umoja wa Afrika katika kuhakikisha kuwa wanaondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika.

Rais Mohammed ameongeza kuwa amani na usalama vitakumbukwa kuwa ni msingi wa maendeleo kwenye katika jamii. Aidha, Rais huyo ameuomba umoja wa Afrika kushirikiana kwa karibu na Somalia katika kuhakikisha kuwa wanatokomeza vikundi vya kigaidi (Alshabab) kwa maendeleo ya ukanda wa Afrika.

Pamoja na mambo mengine, Umoja wa Afrika umekubaliana kuongeza muda wa kuondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika kwa kipindi cha miaka 10 ijayo kuanzia mwaka 2021 hadi 2030.

MENEJIMENTI YA MKOA WA IRINGA YATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI DODOMA

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Happiness Seneda akielezea jinsi Mkoa wa Iringa unavyonufaika na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ofisini kwake.
Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Manyike akielezea fursa za uwekezaji zilizopo Jiji la Dodoma kwa Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa

Na. Dennis Gondwe, IRINGA

KATIBU Tawala Mkoa wa Iringa, Happiness Seneda ameitaka timu yake ya menejimenti kuchangamkia fursa za uwekezaji zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambalo ni makao makuu ya nchi ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Kauli hiyo aliitoa katika kikao cha Menejimenti cha Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo mwishoni mwa wiki.

Seneda alisema kuwa amewakaribisha wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kikao cha Menejimenti ili kuelezea fursa zilizopo jijini Dodoma.

“Serikali imefanya maamuzi mazuri kuhamishia makao makuu Dodoma kwa sababu kumefungua fursa nyingi ambazo hazikuwepo awali. Na sisi tunataka kunufaika na fursa hizo, wawekezaji wa kwanza ni sisi” alisema Seneda. Timu ya wataalam wataelezea fursa za uwekezaji zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuwashawishi kuzichangamkia, aliongeza.

“Ndugu zangu hakikisheni mnawekeza Dodoma, humtajutia sababu fursa nyingi zipo wazi. Unapofanya uwekezaji jijini Dodoma maana yake, wewe unakwenda kutengeneza Masaki ya Dodoma na Posta ya Dodoma. Usije kuona kuwa Dodoma ni mbali, muda mfupi ujao utakuja kujutia. Mfano eneo la Nzuguni litakuja kupaa sana, uwanja wa mpira utajengwa hapo, kituo kikuu cha mabasi kipo Nzuguni, soko kuu la Job Ndugai lipo Nzuguni hilo ni eneo la kimkakati,” alisema Seneda.

Kwa apande wake Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Manyike alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina fursa nyingi za uwekezaji.

“Halmashauri imetenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda mbalimbali katika Kata ya Nala. Eneo la Nala linapatikana barabara kuu ya kwenda Singida umbali wa kilometa 15 kutoka katikati ya Jiji. Eneo hili ni la kimkakati kwa ajili ya viwanda vya aina mbalimbali vikubwa na vidogo” alisema Manyike.

Akifafanua zaidi alisema kuwa maeneo yaliyotengwa ni kwa ajili ya viwanda vya kufua umeme wa upepo, matengenezo ya magari, na viwanda vya Dawa. Vingine ni viwanda vya nguo, viwanda vya vyakula, viwanda vya chuma na viwanja kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya biashara.

Aliongeza kuwa Halmashauri hiyo imepima viwanja kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama ujenzi wa hoteli na nyumba za kupangisha katika maeneo ya Mtumba, Iyumbu, Njedengwa na Kitelela. Fursa nyingine alizitaja kuwa ni ujenzi wa shule na vituo vya afya. “Wote tunafahamu kuwa Jiji linaendelea kukua kutokana na idadi ya watu kuongezeka hivyo kuna fursa za uwekezaji katika ujenzi wa shule kwa ajili ya huduma za elimu. Vilevile, ujenzi wa vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya huduma za matibabu. Viwanja kwa ajili ya matumizi ya shule na hospitali vinapatikana maeneo ya Mtumba, Kikombo, Chahwa na Nala” alisema Manyike.

Kiutawala Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina ukubwa wa kilometa za mraba 2,576, ikiwa na kata 41 na mitaa 222.

DKT.ABBASI: BASATA, BODI YA FILAMU NA COSOTA TOENI MSAADA WA KISHERIA KWA WASANII

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (wakwanza kulia) akizungumza na Wanamuziki wa Injili (hawapo pichani) kuhusu azma ya serikali ya kuendeleza sekta ya sanaa hivyo na kuwataka watoe maoni ya mambo gani yaboreshwe kuendeleza tasnia hiyo, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, kufuatia tamko la Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa kwa wanamuziki wa injili alipokuwa akifungua Bunge.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (aliyeketi watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wasanii wa Muziki Injili waliyohudhuria kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa kundi la wanamuziki wa injili, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kikao hicho.
Msanii wa Muziki wa Injili Boniface Mwaitege akitoa ombi kwa serikali kuwasaidia wasanii wa Muziki wa Injili wanao dhulumiwa haki zao na moja ya kampuni (jina limehifadhiwa) ya usambazaji wa nyimbo za injili njia ya mtandao, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Msanii wa Muziki wa Injili Christina Shusho akitoa ombi kwa serikali la kuandaliwa kwa Tuzo za Muziki wa Injili nchini ili kutoa hamasa kwa wasanii hao, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Mtangazaji wa Kipindi Chomoza kinachotangaza Muziki wa Injili kutoka Televisheni ya Clouds James Temu akitoa ombi kwa serikali la wasanii kupata msaada wa kisheria ili kuwasaidia kupata haki zao kutokana na changamoto za mikataba mingi kuwa ya ulaghai, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Msanii wa Muziki wa Injili Emmanuel Mgaya akitoa ombi kwa serikali la kuangalia suala la gharama za kusajili Youtube Channel kuwa ni kubwa sana kwa kundi la wasanii, kwani wao hutumia akaunti hizo kutafuta masoko ya kazi zao na siyo kuhabarisha umma, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao na Wanamuziki wa Injili kujadili mikakati ya kuendeleza tasnia sekta ya sanaa kufuatia tamko la Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akifungua Bunge.

 

SERIKALI YAENDELEA KUONGEZA MATUMIZI YA TEHAMA KATIKA SHULE ZA UMMA

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dk Zainab Chaula akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi na sekondari jijini Dodoma, jana. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF). (Picha na WUUM)
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dk Zainab Chaula akimkabidhi mmoja wa walimu waliohitimu mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi na sekondari jijini Dodoma, jana. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF). (Picha na WUUM)
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dk Zainab Chaula akimkabidhi mmoja wa walimu waliohitimu mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi na sekondari jijini Dodoma, jana. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF). (Picha na WUUM)
Baadhi wa walimu kutoka shule za msingi na sekondari kutoka Tanzania Bara na Visiwani wakimskiliza Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dk Zainab Chaula wakati wa kufunga mafunzo ya TEHAMA kwa walimu hao jijini Dodoma, jana. (Picha na WUUM)
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) , Justina Mashiba akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi na sekondari jijini Dodoma, jana. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Mfuko wa huo. (Picha na WUUM)

Na Faraja Mpina - WUUM

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ulio chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano) umetoa mafunzo ya TEHAMA kwa walimu 601 wa shule za umma za msingi na sekondari za Tanzania bara na visiwani.

Mafunzo hayo yametolewa katika makundi mawili ambapo walimu 297 wamepata mafunzo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na walimu 304 katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ikiwa ni muendelezo wa Mfuko huo kutoa mafunzo hayo kwa walimu wa umma yaliyoanza kutolewa toka mwaka 2016.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dodoma, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Zainab Chaula amesema kuwa mafunzo hayo ni muendelezo wa utekelezaji wa Sera ya Taifa ya TEHAMA ya mwaka 2003 na marekebisho yake ya mwaka 2016 na Sera ya Elimu ya mwaka 2014 zinazoainisha kuanzisha na kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kuboresha mchakato wa ujifunzaji katika viwango tofauti vya elimu.

“UCSAF imegawa kompyuta mashuleni, walimu mnatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanajua kuzitumia, ndio sababu mmepewa mafunzo ili mkatimize wajibu wenu”, alizungumza Dkt. Chaula

Naye Mtendaji Mkuu UCSAF, Justina Mashiba amesema kuwa mfuko huo umekuwa ukipeleka vifaa vya TEHAMA katika shule za umma pamoja na kutoa mafunzo kwa walimu ili kurudisha heshima katika shule hizo.

Amesema kuwa tangu UCSAF ianze kutoa mafunzo hayo mwaka 2016, jumla ya walimu 2,213 wa shule za msingi na sekondari wamepata mafunzo hayo ili kuwajengea uwezo wa kutumia vifaa vya TEHAMA na kufundishia.

Ameongeza kuwa, UCSAF inaendelea kujipanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili kuendelea kuinua matumizi ya TEHAMA nchini hususani kwa kuwezesha shule za umma.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Elimu Msingi TAMISEMI, Suzan Nusu amesema kuwa walimu waliohudhuria mafunzo hayo walikuwa na vigezo na Wizara itahakikisha mafunzo yaliyotolewa yanatekelezwa kwa vitendo ili kutimiza lengo lililokusudiwa.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano)

 

Act now!!!

$
0
0


Workforce Development & 

Continuing Education 

 GEER Up for Your Future! 

Governor’s Emergency Education Relief Fund 

Have you experienced any of these? 

Lost your job because of COVID? 

Lost hours at work because of COVID? 

Had a hard time finding a new job because of COVID? 

If the answer is yes to any of these, you may be eligible for help! 

Did you know? 

A certificate, license, or credential in a field like healthcare, information technology, or building trades can help you find a job more quickly. With the Maryland Governor’s Emergency Education Relief Fund, you may qualify for help to get that credential, so that you can find a new job more easily or stabilize your current employment.

The Governor’s Emergency Education Relief (GEER) Program can help pay for  

Tuition and fees up to $3500 for approved short-term job training courses at 

Montgomery College that will lead you to a certificate, license, or credential in a 

wide range of job fields 

Technology to help you through online instruction, up to $1000 for approved 

courses that last 18 or more hours. 

Other expenses like books, certification, licensing, or testing fees up to $500 to 

help you get across the finish line 

To qualify, you must 

• Be a Maryland resident 

• Be legally eligible to work in the U.S. 

• Have your employment status affected by COVID – this includes a job loss, 

reduction in hours, unstable employment, or challenges finding new 

employment 

• Meet income eligibility guidelines 

• Not owe any more than $5000 to Montgomery College 

For more information and the application, please visit our webpage at 

GEER Program 

GEER Up for Your Future! 

This $1,361,801 grant, awarded to Montgomery College from the U.S. Department of Education and the Maryland Higher Education Commission, is 100% funded from the Coronavirus Aid, Relief, and Economic Security Act (CARES Act) Education Stabilization Fund Program - Governor’s Emergency Education Relief (GEER) Fund. CFDA 84.425C.

 Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Business & Professional 

Next Course Date

Certified Internal Auditor 

MGT593 – Certified Internal Auditor Part 1: Essentials 

MGT594 – Certified Internal Auditor Part 2: Practice of Internal Auditing MGT595 – Certified Internal Auditor Part 3: Business Knowledge for Internal Auditing

1/26 

3/02 

4/06

Coaching Certification 

MGT488 – Introduction to Coaching 

MGT502 – Coaching Clinic, Intro 

Practicum 

Mastery

02/06 

02/20, 02/23 

TBD 

TBD

Income Tax Preparer 

TAX003 – Income Tax Preparation 

TAX002 – Individual Tax Preparer Exam Test Prep

1/05 

TBD

Real Estate Appraiser 

REC175 – Basic Appraisal Principles 

REC176 – Basic Appraisal Procedures 

REC069 – Real Estate: Appraisal Standards/Ethics

1/09 

2/06 

03/13

Real Estate Sales 

REB010 – Basic Real Estate Principles and Practices 

REB142 – Real Estate Basic Principles Retest

1/21, 2/02 

1/13, 3/8, 3/10, 4/28

Human Resources: Society for Human Resource Management  

MGT603 – SHRM CP/SCP Certification Prep 

MGT430 – SHRM Learning System for Certification Preparation

2/15, 2/19 

TBD



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 1

Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Information Technology 

Next Course Date

Cloud Computing: Amazon Web Services Certified Solutions Architect Certification ITI443 – AWS: Amazon Web Services I 

ITI444 – AWS: Amazon Web Services II 

ITI445 – AWS: Amazon Web Services III

3/02 

03/23 

04/13

Cloud Computing: Microsoft Azure Certification 

ITI356 – Microsoft Azure 

02/09

Database: Microsoft Azure Data Base Administration 

ITI468 – Microsoft Azure Data Base Administration 

04/05

Salesforce: Certified Salesforce Administrator and Salesforce Platform App Builder ITI438 – Salesforce Fundamentals 

ITI370 – Salesforce Administrator Training

02/02 

02/23, 3/23

Computer Networks: CompTIA® Network+ Certification 

ITI241 – Network+ Certification Training and Test Prep 

 OR 

ITI294 – ITI Networking Academy (also includes IT Fundamentals  Certification)

02/22 

02/01

Cybersecurity - CompTIA® Security + Certification 

ITI375 – Cybersecurity Foundation Training 

 OR 

ITI240 – Security + Certification and Test Prep 

 OR 

ITI294 – ITI Networking Academy (also includes IT Fundamentals  Certification)

02/02 

02/06 

02/01

The Certified Information Systems Security Professional (CISSP) 

ITI380 – CISSP Training 

03/02

Database Administration: Oracle Certified Associate 

ITI212 – Oracle 12c: Intro to SQL 

ITI215 – Oracle 12c: Database Administrator Certified Associate

TBD 

TBD

Data Analysis: Tableau Desktop Specialist Certification 

ITI420 – Mastering Tableau 

3/23

Computer Repair and Help Desk (CompTIA® A+ Certification) 

TTG580 – A+ 220-1001 Exam Prep: Core 1 

TTG581 – A+ 220-1002 Exam Prep: Core 2

3/29 

1/04, 3/29



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 2

Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Public Safety 

Next Course Date

CDL (Truck License) 

2/16, 3/22, 4/26

911 Dispatcher 

TBD

Special Police Officer 

TBD

Education & Personal Services 

Next Course Date

Alternative Certification for Effective Teachers 

Intensive cohort program with separate application 

TBD

Nail Technician 

COS004 – Nail Technician I 

COS005 – Nail Technician II 

COS006 – Nail Technician III

TBD 

01/04 

03/08

MSDE: 90 Hour Child Care Training (Preschool) 

ECH205 – Child Growth and Development 

ECH207 – Planning Curricula for Child Care 

ECH170 – Communications Skills for Child Care Professionals 

ECH271 – Including All Children and the ADA 

ECH292 – Supporting Breastfeeding 

ECH305 – Health and Safety 

CPR090 – CPR/AED & Basic First Aid

1/16, 1/19 

3/23, 3/27 

4/19 

2/10 

TBD 

2/27 

04/17

MSDE: 90 Hour Child Care Training (Preschool) - Spanish 

ECS023 – Crecimiento y desarrollo infantil 

ECS027 – Planificación de currículos para centros de Cuidado infantil ECS042 – Técnicas de comunicación 

ECS082 – Integrando a niños con discapacidades en el aula 

ECS100 – Lactancia 

ECS110 – Salud y seguridad  

ECS 086 Primeros auxilios y RCP para profesores de educación preescolar

1/16, 1/20 

3/27, 3/31 

2/22 

4/27 

TBD 

03/06 

TBD

MSDE: 90 Hour Child Care Training (Infant and Toddlers) 

ECH205 – Child Growth and Development 

ECH208 – Infant and Toddler Development and Curriculum Planning ECH170 – Communications Skills for Child Care Professionals 

ECH271 – Including All Children and the ADA 

ECH292 – Supporting Breastfeeding 

ECH305 – Health and Safety 

CPR090 – CPR/AED & Basic First Aid

  

1/16, 1/19 

TBD 

4/19 

2/10 

TBD 

2/27 

4/17



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 3

Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Education & Personal Services (continued) 

Next Course Date

MSDE: 90 Hour Child Care Training (Infant and Toddlers) – Spanish ECS023 – Crecimiento y infantil 

ECS049 Desarrollo y planificación de currículos para bebés 

ECS042 – Técnicas de comunicación 

ECS082 – Integrando a niños con discapacidades en el aula 

ECS100 – Lactancia 

ECS110 – Salud y seguridad  

ECS 086 Primeros auxilios y RCP para profesores de educación preescolar

1/16, 1/20 

TBD 

2/22 

4/27 

TBD 

03/06 

TBD

Family Child Care 

ECH294 – Sudden Infant Death Syndrome 

ECH172 – Emergency Preparedness Training 

ECH257 – Medication Administration Training 

ECH271 – Including All Children and the ADA 

ECH292 – Supporting Breastfeeding 

ECH305 – Health and Safety 

CPR090 – CPR/AED & Basic First Aid 

Pick One: 

ECH197 – Family Child Care; Pre-service module series 

 OR 

MSDE: 90 Hour Child Care Training

02/18 

04/24 

2/20, 04/03 

02/10 

TBD 

02/27 

4/17 

Call Dept

Family Child Care – Spanish 

ECH294 – Sudden Infant Death Syndrome 

ECS063 – Preparación para emergencias 

ECS069 – Administración de medicamentos 

ECS082 – Integrando a niños con discapacidades en el aula 

ECS100 – Lactancia 

ECS110 – Salud y seguridad  

ECS 086 Primeros auxilios y RCP para profesores de educación preescolar 

Pick One:  

ECS047 – Abra su guardería en casa 

 OR 

MSDE: 90 Hour Child Care Training

02/18 

TBD 

02/13, 04/10 

04/27 

TBD 

03/06 

TBD 

Call Dept

MSDE: Child Development Associate (CDA) 

ECH205 – Child Growth and Development 

ECH132 – Child Development Associate (CDA) Credential Assessment  Preparation 

Pick One:  

ECH207 – Planning Curricula for Child Care  

 OR 

ECH208 – Infant and Toddler Development and Curriculum Planning

1/16, 1/20 

TBD 

3/23, 3/27, 3/31



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 4

Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Education & Personal Services (continued) 

Next Course Date

MSDE: Child Development Associate (CDA) - Spanish 

ECS023 – Crecimiento y desarrollo infantil 

ECS028 – Preparación para la credencial de desarrollo infantil 

 Pick One:  

ECS027 – Planificación de currículos para centros de cuidado infantil  OR 

ECS049 Desarrollo y planificación de currículos para bebés

1/16, 1/20 

TBD 

3/27, 3/31 

TBD



Technical/Trades 

Next Course Date

Certified Energy Photovoltaic Associate 

TTG521 – Solar PV Design and Installation 

1/26

EPA 608 - CFC Certification  

TTG373– Fundamentals of Refrigeration 

TTG375 – HVAC Technician Development

1/28, 2/01 

1/26, 4/26

Home Improvement Contractor 

SMB181 – Home Improvement 

HBI195 – Home Improvement (Spanish)

1/11, 2/22, 4/12 

1/09, 2/27

Home Inspector 

SMB322 – Home Inspection: Make It Your Business 

SMB967 – Home Inspection: Continuing Education Pt. 1 

SMB968 – Home Inspection: Continuing Education Pt. 2

1/21, 1/23 

2/03 

3/24

OSHA 500 Trainer course Occupational Safety and Health for the Construction  Industry 

TBD

OSHA 510 Occupational Safety and Health for the Construction Industry 

TBD

OSHA 511 Occupational Safety and Health Standards for General Industry 

TBD

OSHA 7300 Understand OSHA’s Permit-Required Confined Space Standard 

TBD

OSHA 7845 Recordkeeping Rule 

TBD



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 5

Montgomery College 

GEER Program Approved Courses  

Health Sciences 

Next Course Date

Basic Cardiac Life Support for Healthcare Providers 

CPR007 – Basic Cardiac Life Support for Healthcare Providers 

3/27, 4/3, 4/29

CPR/AED & Basic First Aid 

CPR090 - CPR/AED & Basic First Aid 

04/17

Certified Nursing Assistant (CNA) 

NUR070 – Hospital-based Certified Nursing Assistant 

NUR071 – Hospital-based CNA Clinical

1/24, 1/26 

3/23, 3/28

Certified Nursing Asst. (CNA) & Geriatric Nursing Asst.(GNA) 

AHT028 – Certified Nursing Assistant (nursing homes) 

AHT223 – Clinical Hours for CNA (nursing homes)

1/19, 1/20, 2/1, 3/22 

2/22, 3/11,3/31,4/21

Clinical Medical Assistant 

HHS112 – Clinical Medical Assistant (classroom) 

HHS126 – Clinical Medical Assistant (clinical)

2/15, 2/16 

2/22,2/23, 2/24, 2/25

Medicine Aide 

AHT145 – Medicine Aide Update 

1/16, 2/13, 3/13

Nurse Refresher 

NUR057 – Nurse Refresher - Face to Face 

NUR069 – Nurse Refresher – Online 

 (Either class must take the following two courses) 

NUR023 – Nursing Lab 

NUR007 – Nurse Refresher: Clinical

1/20, 1/23 

1/25, 2/06 

03/06, 03/13 

3/8, 3/10,3/23

Pharmacy Technician Certificate 

HHS105 – Pharmacy Technician 

02/08, 02/13

EKG Technician Exam Preparation 

HHS051 – EKG Technician 

02/16

Phlebotomy Technician 

HHS034 – Phlebotomy Technician 

HHS115 – Phlebotomy Technician - Clinical

2/15, 2/22 

3/01



Approved GEER Courses Rev. 11.30.20. 6


Viewing all 45987 articles
Browse latest View live
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>