Quantcast
Channel: VIJIMAMBO
Viewing all 45921 articles
Browse latest View live

RC GAMBO: SERIKALI ITAYAPA KIPAUMBELE MAMBO YA MSINGI ILI KUONDOA CHANGAMOTO KWA JAMII

$
0
0
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Mashaka Gambo akiingia ukumbini tayari kwa kuanza rasmi kwa kongamano na waandishi wa habari na wadau mbalimbali wa maendeleo katika mkoa wa Arusha. Picha na Vero Ignatus Blog. 
Mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Gabriel Daqqaro akizungumza na waandishi wa habari na wadau wa maendeleo katika komgamano hilo.
Mkurugenzi wa Kituo cha mikutano cha kimataifa AICC Elishilia Kaaya akizungumza na wadau mbalimbali waliohudhuria katika kongamano hilo na yeye kama mwenyeji wa eneo hilo akiwakaribisha katika kituo hicho.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano ambalo aliwaahidi waandishi kuwa ataliiitisha kwaajili ya kujadili na kupata taarifa ya maendeleo katika mkoa wa Arusha pamoja na wadaumbalimbali.
Mwenyekiti wa Arusha press club (APC) Akizungumza na katika kongamano hilo.
Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha Richard Kwitega akizungumza katika kongamano hilo.
Wa kwanza kushoto ni Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo ,akiwa kwenye kongamano katika kituo uliofanyika katika kituo cha kimataifa cha mikutano AICC katika ukumbi wa Mbayuwayu.
Wadau wa Utalii kutoka TANAPA wakiwa katika kongamano la wadau wa habari mkoa wa Arusha.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika kongamano hilo lililoitishwa na mkuu wa mkoa wa Arusha ili kuangalia na kujadili maendeleo ya mkoa kwa ujumla.
Wa kwanza kushoto ni mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi Mussa Juma ,akifuatiwa na Omary Moyo wakiwa katika kongamano hilo.
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa pamoja na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari waliohudhuria kongamano hilo.
Mwandishi wa habari wa kituo cha luninga cha chanel Ten Jamillah Omary akiwa na mkurugenzi mwenza wa Me Production ambaye pia ni mpiga picha wa kituo cha luninga cha ITV Anold Rweyemamu.
Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athuman Kihamia,aliyeko kushoto kwake ni nyekiti wa ccm mkoa ndugu Laizer 
Na.Vero Ignatus, Arusha.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mashaka Mrisho Gambo amefungua Kongamana kutoa taarifa ya maendeleo katika mkoa wa Arusha ambapo kongamano hilo limewashirikisha wadau wa habari katika kuangalia na kutafakari na kupitia pamoja na kuangalia mpango mkakati wa maendeleo katika mkoa.

Gambo amesema kuwa kongamano hilo lina lengo la kutoa mrejesho kwa Watanzania kupitia waandishi kwa kipindi cha miezi sita ,na kuangalia mambo gani serikali ikiyapa kipaumbele itaondoa changamoto mbalimbali katika jamii kwa ujumla.

Aidha amesema kuwa utekelezaji wa shughuli za kiserikali katika mkoa wa Arusha kwa kipindi cha miezi sita hadi kufikia desemba 2016 umekuwa na mafanikio makubwa ,ambapo amesema kuwa hii ni kutokana na utamaduni wa kufanya na kutekeleza majukumu ya kazi kwa vitendo.

Amesema utekelezaji huo umechangia katika kuboreka kwa maeneo mbalimbali ya sekta muhimu katika kukuza uchumi katika mkoa hasa pato la mkoa na wananchi moja kwa moja.

“Katika kipindi hiki,miradi mingi ya maendeleo imetekelezwa na kupewa kipaumbele cha kutosha hivyo kwa namna moja kutekeleza mkakati wa Taifa wa kukuza uchumi na kuondoa umaskini (MKUKUTA II)katika mkoa na taifa kwa ujumla”alisema Gambo.

Amesema kuwa Mkoa umesimamia utekelezwaji wa shughuli za serikali na kushuhudia mafanikio katika sekta za kilimo,afya,maji,barabara,mofugo,maliasili na nyinginezo kama takwimu zilivyowasilishwa .

Amesema kuwa serikali imejipanga kuhangaika na wale wote ambao wanachochea migogoro kwa wananchi na kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi hatutawafumbia macho.

Kwa upande wamafanikio utekelezaji wa mkoa kuanzia mwaka 2005 mkoa ulikuwa na shilingi 723,809 milioni kwa mwaka huo mkoa ulikuwa wa (9) katika kuchangia patao la Taifa,ambapo pato la mkazi lilikadiriwa kuwa shilingi 506,902 kwa mwaka sawa na shilingi 1,389 kwa siku.

Kwa mwaka 2010 pato la mkoa wa Arusha lilikuwa shilingi 2,136,514milioni kwa kuchangia pato la taifa Arusha ilikuwa ya 7.mwaka huo pato la mkazi wa Arusha lilikuwa shilingi 1,283,361 kwa mwaka sawa na shilingi 3,516 kwa siku.

Hadi mwaka 2015 pato la mkoa linakadiriwa kuwa shilingi 4,271,447milioni.
kwa takwimu hizo pato la mkazi wa Arusha lilikuwashilingi 2,322,031 milioni kwa mwaka ni sawa na shilingi 6,361 kwa siku.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MARAIS MBALIMBALI WA AFRIKA KATIKA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA AFRIKA (AU) MJINI ADDIS ABABA ETHIOPIA

$
0
0
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika moja ya Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa kwa ajili ya mazungumzo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mazungumzo katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kumaliza mazungumzo yao katika moja ya katika Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Misri Abdel Fattah El Sisi kabla ya kuanza mazungumzo yao katika moja ya Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
  Rais wa Misri Abdel Fattah El Sisi akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya mazungumzo yao katika moja ya Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Misri Abdel Fattah El Sisi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao katika moja ya Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Misri Abdel Fattah El Sisi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao katika moja ya Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kwenye mazungumzo yake pamoja na Rais wa Misri Abdel Fattah El Sisi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Akinwumi Adesina mara baada ya kumaliza mazungumzo yao mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni kabla ya kuanza mazungumzo yao katika moja ya Ofisi za AU mjini Addis Ababa Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni kabla ya kuanza mazungumzo yao rasmi katika moja ya Ofisi za AU mjini Addis Ababa Ethiopia.
. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn wakati akitoka kwenye mkutano wa AU mjini Addis Ababa nchini Ethiopia. 

PICHA NA IKULU

CUF YA PROFESA LIPUMBA YAJIBU MAPIGO KUHUSU RUZUKU WALIYOPEWA NA HAZINA

$
0
0

Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi (Taifa) wa Chama cha Wananchi (CUF), Thomas D.C Malima (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam leo kuhusu ruzuku ya chama hicho iliyopokelewa kupitia akaunti namba 2072300456 ya Benki ya NMB Tawi la Temeke. Kulia ni Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Mneke Jafar na Katibu Jumuiya ya Wanawake (JUKE), Salama Masoud.
Meza Kuu. Kutoka kulia ni Kamanda Mkuu, Athumani Hamadi,Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Mneke Jafar, Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi (Taifa) wa Chama cha Wananchi (CUF), Thomas D.C Malima, Katibu Jumuiya ya Wanawake (JUKE), Salama Masoud na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, Masha Amour.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano ukiendelea.


The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) chini ya Uongozi thabiti wa Mwenyekiti wake Mhe Profesa Ibrahim Haruna Lipumba kinaishukuru na kuipongeza Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa kwa kukipatia Chama chetu Ruzuku yake inayopatikana kwa Mujibu wa Sheria ya vyama vya Siasa Namba 5 ya mwaka 1992.

Pamoja na Ruzuku ya CUF kuzuiwa kwa Muda wa miezi mine (4) kuanzia mwezi Septemba, 2016 hadi Desemba 2016 kutokana na sintofahamu ya uongozi wa Kitaifa wa CUF, Msajili hakuona haja ya kuendelea kuizuia wakati shughuli za chama zinafanyika kila siku. Kuendelea kuizuia Ruzuku halali ya chama ni kukizuia kufanya kazi zake halali za kisiasa ikiwa ni pamoja na kushiriki katika chaguzi mbali mbali za kiserikali zinazoendelea nchini. 

Waheshimiwa wanahabari, Baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa kupitia katiba ya CUF ya mwaka 1992, Toleo la 2014 alijiridhisha kuwa Mhe Profesa Ibrahim Haruna Lipumba ndiye Mwenyekiti halali wa CUF kwa kuwa mchakato wa kukamilisha kujiuzulu kwake haukukamilika kabla yeye kutengua barua yake ya kujiuzulu.

Mnamo Tarehe 23 Septemba 2016 , Msajili aliandika barua kwa Katibu Mkuu wa CUF kumjulisha msimamo na mwongozo wa wake  kuwa  “Mwenyekiti wa Taifa wa CUF ni  Mhe Profesa Ibrahim Haruna Lipumba”

Baada ya Katibu Mkuu kupokea barua hiyo aliamua kupinga Uamuzi huo wa Msajili wa Vyama vya Siasa uliotokana na Malalamiko ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wapatao 324 kati ya 343 ambao walilalamikia uvunjifu wa Katiba ya CUF unaofanywa na Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad kwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Maaalim Seif na timu yake walienda mbali kwa “kuikimbia ofisi yake” iliyoko hapa Ofisi Kuu ya CUF Buguruni na kukimbilia Mafichoni kusikojulikana na kusababisha kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kiutendaji.  Hivyo, Mwenyekiti wa Taifa aliamua kufanya mabadiliko ya Kurugenzi za Chama kwa kumujibu wa ibara ya 91(1)(f) ya katiba ya CUF, nainukuu:

“Mwenyekiti wa Taifa atateua kutoka miongoni mwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa, wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa au wanachama wajasiri kuwa wakurugenzi na manaibu wakurugenzi wa Chama pamoja Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama baada ya kushauriana na Makamu Mwenyekiti na kufikisha uteuzi huo mbele ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa kuthibitishwa”. 

Kwa mujibu wa Ibara ya 95(3) ya Katiba ya CUF ya mwaka 1992, Toleo la 2014, Nainukuu:-
  “Naibu Katibu Mkuuatakayemfuatia Katibu Mkuu kwa madaraka ni Yule anayetoka upande tofauti wa Jamhuri ya Muungano na upande anotoka Katibu Mkuu”.  Kwa kifungu hicho, Katibu Mkuu anaposhindwa kutekeleza majukumu yake kwa sababu yoyote ile, Naibu Katibu Mkuu Bara ndiye anakaimu Ukatibu Mkuu mpaka atakaporejea ofisini kuendelea na majukumu yake.

Hii inatokana ukweli wa kikatiba uliowekwa kwenye ibara ya 105 (1) ya Katiba ya CUF ya mwaka 1992, Toleo la 2014, Nainukuu:-
  
 “Pale ambapo mwanachama yeyote wa Chama mwenye madaraka kwa mujibu wa masharti ya katiba hii, kwa sababu yeyote ile, hawezi kutekeleza kazi zake kwa muda, mwanachama anayemfuata kwa madaraka kwa mujibu wa katiba atakaimu nafasi yake”. 

Hivyo, kwa mujibu wa ibara hii na ile ya 95(3) Ni suala la kikatiba lisilo na shaka kwa Mheshimiwa Magdalena Sakaya (Mb) ambaye ndiye anayemfuata Katibu Mkuu kwa Madaraka kukaimu ofisi ya Katibu Mkuu mpaka atakaporejea ofisini kwake Buguruni. Kwa hiyo, Mhe Sakaya ataendelea kufanya majukumu yote ya Katibu Mkuu kwa mujibu wa Katiba ya CUF. Na Katibu Mkuu hapaswi kulalamika.

Kuhusu masuala ya fedha, Kwa mujibu wa kanuni ya jfedha ya mwaka 2014, ibara ya 22(2)(a) (B):-“Masuala yote ya fedha yanasimamiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi na ndiye Mshauri Mkuu wa Katibu Mkuu kuhusu Masuala ya Fedha”. 

Na kwa kuwa Katibu Mkuu ni Ofisi siyo mtu, anapokuwa hayupo ofisini Naibu Katibu Mkuu Bara atatekeleza majukumu yote ya ofisi ya Katibu Mkuu kama Kaimu Katibu Mkuu.  Ni aibu kwa Mwalimu Seif kulalamika wakati anaijua katiba ya CUF na anajua kuwa amekimbia ofisi mwenyewe ndiyo maana Mhe Sakaya anafanya kazi alizozikimbia kwa kushirikiana na wakurugenzi walioteuliwa na Mwenyekiti wa Taifa kwa mujibu wa Katiba.

Waheshimiwa wanahabari, Chama Chetu kimepokea sehemu ya malimbikizo ya ruzuku ya CUF Kiasi cha Tsh. 369,366,671/=. Tumepokea Ruzuku hiyo kupitia Akaunti namba 2072300456 ya The Civic United Front (CUF-Chama cha Wananchi)  NMB Tawi la Temeke. Hii siyo akaunti Mpya ya Chama kama inavyodaiwa Maalimu Seif na genge lake.

Akaunti hii ilifunguliwa zaidi ya miaka Kumi iliyopita na Katibu Mkuu kwa ajili ya kupokea na kutoa fedha za CUF kwa wilaya ya Temeke. Na kwa mujibu wa Kanuni ya Fedha ya CUF ya mwaka 2014, ibara ya 23(1)(f) Nainukuu: -
  
“Chama ngazi ya Taifa kinaweza kufungua akaunti tofauti au kubadili matumizi ya akaunti iliyopo kwa ajili ya kazi au shughuli maalum kadri itakavyoona inafaa. Akaunti hizo zilizofunguliwa utawekwa utaratibu maalum wa kuzihudumia”.

Kwa kuzingatia hali iliyopo, Tuliona kubadilisha matumizi ya Akaunti ya The Civic United Front (CUF-Chama cha Wananchi), Tawi la Temeke itumike kupokelea Ruzuku ya Chama toka serikalini ili iweze kufikia katika mikono salama kwa ajili ya uendeshaji wa Shughuli za Chama.

Waheshimiwa wandishi, Baada ya kuipokea Ruzuku hiyo, tayari tumeshaitumia katika harakati za Kiuchaguzi katika Chaguzi za marudio ya Udiwani katika kata 14 ambapo CUF imefanya vizuri sana katika kata tatu (3) ambazo ni Nkome (Geita), Malya (Kwimba) na Kijichi (Temeke). 

Waheshimiwa wandishi, Ikumbukwe kuwa Tangu  Mwalimu Seif na Genge lake wakimbie Ofisi Kuu Buguruni Tarehe 23 Septemba 2016, shughuli za chama zilikuwa zikiendelea kufanyika japokuwa hatukuwa tunapata ruzuku toka Serikalini. Wanachama wetu walikuwa na ari zaidi ya kukichangia chama ili kuendeleza harakati za ukobozi wa Haki sawa kwa Wote. Kwa mapenzi makubwa ya Chama chake Mheshimiwa Mwenyekiti wetu Profesa Ibrahim Haruna Lipumba alikuwa Msitari wa mbele kukisaidia chama kwa kujitolea na hata kukikopesha chama ili tutekeleze Majukumu ya ujenzi wa chama.

Waheshimiwa wanahabari, Hii si mara ya kwanza Mhe Profesa kukisaidia chama Chetu. Ipo mikataba kadhaa ambayo Mwenyekiti wetu amewahi kukikopesha chama fedha zake mwenyewe.

Waheshimiwa wandishi, Ni jambo la kusikitisha kuwa kwa takribani mwaka mmoja hasa baada ya Mhe Profesa Lipumba kuwa nje ya uenyekiti wa Taifa wa CUF, Wilaya zote za Tanzania Bara zilisitishiwa Ruzuku toka Ofisi kuu wakati wilaya zote za Zanzibar zikiwa zinaendelea kupokea ruzuku. Kwa kweli huu ni uonevu mkubwa kwa wanaCUF wa Tanzania Bara na huu ni mpango wa Makusudi wa Maalim Seif na genge lake.

Baada ya kupokea Ruzuku hiyo, Tumeamua kuzipelekea ruzuku Wilaya zote za Tanzania Bara alau ruzuku ya miezi mitatu mitatu kwa kila wilaya. Mpaka sasa tumeshatuma ruzuku katika wilaya 82 ambapo Tsh. 66,300,000/= zimetumika. 

Ikumbukwe kuwa Wilaya zinazotakiwa kupokea ruzuku ni wilaya zote zilizofanya uchaguzi wa ndani ya Chama ambapo Jumla ya wilaya 104 zina uongozi halali wa chama. Kwa mantiki hiyo, wilaya 22 bado hazijapewa Ruzuku kutokana na matatizo mbalimbali ikiwemo Akaunti zao kuwa dormat kwa muda mrefu, na nyingine kutowasilisha akaunti namba zao ofisini. 

Hivyo, tunatoa wito kwa viongozi wa Wilaya zote wa CUF kwenda benki kuangalia taarifa ya fedha ya akaunti zao kisha kutupa taarifa. Lakini pia ni wajibu wao kufanya matumizi ya fedha hizo kwa mujibu wa sheria za nchi na kanuni ya Fedha za CUF kwa kuwa hizo ni fedha za umma.

Waheshimiwa wandishi, tumesikitishwa na tamko la inayojiita Bodi ya wadhamini ya CUF eti fedha zimeibwa na wanazuia viongozi wa wilaya wasichukue fedha zilizoko kwenye akaunti zao. Kwa mujibu wa ibara ya 98(1) nainukuu:- 

“ Kutakuwa na Bodi ya wadhamini itakayoteuliwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa mujibu wa sheria za nchi kwa kipindi cha miaka mitano (5) na mjumbe anaweza kuteuliwa tena baada ya muda kumalizika”. 

Ndugu wandishi, Bodi ya CUF iliteuliwa kwa mara ya mwisho Januari 2010, hivyo ilimaliza muda wake Januari 2015.  Haijawahi kuteuliwa tena na haijawahi kulipiwa Mchango wa kila mwaka RITA tangu 2013. Kutokana, sheria za nchi na katiba ya CUF, Bodi hiyo ni mfu kwa hiyo haina uwezo wa kushughulikia na kusimamia masuala yoyote ya fedha za CUF. How can a dead body talk about financial matters?. 

Wakiwa wanajua ukweli huo, bado wanakubali kutumika kwa maslahi ya Maalim Seif. Hii ni kuthibitisha kuwa “Mbwa mzee hafundishwi mbinu mpya za kuwinda”. Ni kweli Maalim Seif, Bashange na Katau wamezeeka, ni sawa mbwa wazee wasioweza kutumia mbinu mpya za kujijenga kwa wanachama wa CUF bali wanazidi kujifedhehesha. 

Ndevu zao ni ishara ya kupitwa na wakati. Ni bora watuachie vijana tujitanabahishe kwa mbinu za kisasa za kuiweka kweli ndani ya CUF na Watanzania kwa ujumla. Kama Maalim Seif alikuwa simba wa vita vya miaka 1980, kamwe hawezi kuwa simba wa vita ya 2016/2017. Huwezi kuwa Katibu Mkuu ambaye unapeleka Ruzuku Zanzibar kupitia Michango ya Wabunge lakini ukawa hutaki Wilaya za Tanzania Bara zipate Ruzuku. Huu ni ubaguzi uliokithiri na sisi hatutaukubali.

Tunaiomba ofisi ya Gavana wa Benki kuu kutupilia mbali ombi la Bodi ya wadhamini ya CUF isiyo halali kwa kuwa imepitwa na wakati na inakiuka hata katiba ya CUF ibara ya 98(1) na (2) inayotaka bodi iundwe na jumla ya wajumbe 9 ambapo 3 kati yao lazima wawe wanawake lakini bodi feki ya Mwalimu Seif ina wanaume watupu ndiyo maana wanailalamikia RITA eti wametoa siri za ufeki wao. 

Na kama wanahisi RITA wameghushi nyaraka, waende Polisi wakafungue mashitaka dhidi ya RITA, japokuwa nalo ni jambo gumu kwao maana wao ni Bodi mfu, hawana uwezo wa kushitaki wala kushitakiwa.

Waheshimiwa wanahabari, kwa sasa Maalim Seif anamlaumu kila mtu. Anamlaumu Jaji Mutungi kwa kusema ukweli, anawalaumu Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kwa kuupinga udikiteta wake Mkutanoni, anamlaumu Gavana wa Benki, anailaumu RITA, anamlaumu Jaji Kihiyo, anamlaumu Rais Shein, anamlaumu Jecha, anamlaumu Profesa Lipumba eti anakuja kuzuia asipewe urais wa Zanzibar lakini cha ajabu hajilaumu mwenyewe kwa udikiteta wake ndani ya CUF na tamaa yake ya kupenda fedha za Lowasa kuliko utu na thamani yake kwa jamii.

Mwisho, tunamtaka Mwalimu Seif na Genge lake waende kwa amani watuachie CUF yetu. Hata Mapalala ailianzisha CUF lakini alipoonekana anaisaliti aliamua kuiacha CUF kwenye mikono salama. “Yeye sasa ni Simba mzee hawezi mawindo ya wakati huu”.

Imeandaliwa na;-
Thomas D.C Malima
Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi (Taifa)

KAULI YA SERIKALI BUNGENI DODOMA KUHUSU MWENENDO WA HALI YA UCHUMI WA TAIFA

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwasilisha kauli ya Serikali kuhusu Mwenendo wa Hali ya Uchumi wa Taifa, Bungeni Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (Katikati) akitoka nje ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, baada ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kuwasilisha kauli ya Serikali kuhusu Mwenendo wa Hali ya Uchumi wa Taifa, Bungeni Mjini Dodoma.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakibadilishana mambo mawili matatu, baada ya kumalizika kwa shughuli za Bunge Mchana Mjini Dodoma (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)

MWANAHALISI WAMUOMBA RADHI MHE. RAIS MAGUFULI

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UFARANSA NCHINI NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA CUF PROFESA LIPUMBA KWA NYAKATI TOFAUTI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Malika Berak (kushoto), ofisini kwake, Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza kwa makini Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Malika Berak wakati wa mazungumzo yao yaliofanyika ofisini kwake, Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Malika Berak (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Serikali ya Ufaransa kupitia Benki ya Maendeleo ya Nchi hiyo (AFD) imeahidi kuwa inampango wa kuipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu kutoka wastani wa euro milioni 50 hadi euro milioni 100 kwa mwaka katika miaka ijayo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Malika Berak ametoa kauli hiyo Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na Kufanya mazunguzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuhusu hatua zilizofikiwa katika uandaaji wa kongamano la uwekezaji litakalofanyika Jijini Dar es Salaam kuanzia mwanzoni mwa mwezi Aprili mwaka huu.

Balozi huyo amesema mkopo huo itaiweza na kuisaidia Tanzania kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi hasa katika sekta za maji na usafi wa mazingira na miradi ya umeme.

Kuhusu uandaaji wa kongamano la uwekezaji nchini, Balozi Malika Berak amemweleza Makamu wa Rais kuwa maandalizi ya kongamano hilo kubwa la Kibiashara linalolenga kujenga na Kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Ufaransa yanakwenda vizuri.

Balozi huyo amesema kuwa kongamano hilo ambalo litakuwa la Kikanda litajadili kwa kina fursa za uwekezaji hapa nchini hasa kwenye maeneo ya nishati, usafirishaji, teknolojia ya habari na Mawasiliano na miradi ya maendeleo.

Balozi Malika Berak amemhakikishia Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan kuwa kongamano hilo la kibiashara litawakutanisha pamoja wafanyabiashara Watanzania na wenzao wa Ufaransa katika kujadili na kubadilisha uzoefu katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kibiashara kama hatua ya kuimarisha shughuli zao za kiuchumi.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameipongeza Serikali ya Ufaransa kupitia kwa balozi wake hapa nchi kwa ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika sekta ya maji na usafi wa mazingira, nishati na mapambano dhidi ya umaskini nchini.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amemhakikishia Balozi wa Ufaransa hapa nchini Malika Berat kuwa Tanzania itaendelea kudumisha na kuendeleza mahusiano yaliyopo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa pande Mbili yaani Tanzania na Ufaransa.

Makamu wa Rais pia amepongeza jitihada za Serikali kupitia Ubalozi wake hapa nchini za kuona umuhimu wa kuandaa Kongamano la kibiashara hapa nchini ambalo litatoa fursa kubwa kwa watalaamu wa sekta mbalimbali nchini kukutana na kujadiliana mambo kadhaa ikiwemo fursa za uwekezaji nchini.

Amesisitiza kuwa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakt John Magufuli inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini kwa kupambana na vitendo vya rushwa kama hatua ya kuhamasisha wawekezaji wengi kuja kuwekeza hapa nchini.

Makamu wa Rais amemweleza Balozi wa Ufarana hapa nchini kuwa milango ya ofisi yake ipo wazi muda wote hivyo kama watakwama sehemu yeyote katika kuandaa kongamano hilo amfahamishe haraka ili aweze kuchukua hatua haraka kusaidia mchakato huo kutokana na muhimu wa kongamano hilo hasa wakati huu ambapo Tanzania inataka kujenga uchumi wa viwanda nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba alipomtembelea ofisini kwake, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo.


JUMIA TRAVEL YAJIKITA KATIKA UTALII

$
0
0



Na Jumia Travel Tanzania

Mwaka wa 2016 ulikuwa wenye mafanikio makubwa kwa sekta ya utalii duniani ambapo kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UNWTO), watu bilioni 1.2 walisafiri duniani huku waliotembelea Afrika wakiwa milioni 58.

Taarifa hiyo ilitolewa katika mkutano wa nane uliondaliwa wa INVESTOUR Januari 19, 2017 jijini Madrid nchini Hispania, kwa ushirikiano wa UNWTO na Casa Afrika ambao uliwakutanisha wadau na mawaziri zaidi ya 20 wa utalii kutoka barani Afrika.   

Ajenda kuu za mkutano huo zilikuwa mbili ambazo ni; ‘Tekinolojia na uundaji wa bidhaa mpya za kitalii’ pamoja na ‘Kuendeleza uwezo kwa vijana na wanawake katika utalii.’

Akiwa na mmojawapo wa washiriki waliounda jopo la wazungumzaji katika mkutano huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumia Travel, Bw. Paul Midy alibainisha kwamba, “Idadi kubwa ya wasafiri wa ndani ni ishara nzuri kwamba watu wanavutiwa na vivutio walivyonavyo. Zinahitajika jitihada za wadau wa utalii katika kuwaelimisha na kuvitangaza vivutio hivyo huku tukiwarahisishia miundombinu kama vile malazi ambayo huwezi kuiweka kando pindi unapozungumiza usafiri na utalii. Naamini kwa gharama za malazi kupunguzwa, watu wengi watahamasika kusafiri kwani mahali zilipo hizo hoteli ndipo vivutio vilipo.”


Kwa mujibu wa ripoti hiyo kuna fursa kubwa kwa utalii wa ndani kwa sababu mbali na idadi ya watu bilioni 1.2 waliosafiri duniani, watu bilioni 6 walifanya utalii wa ndani. Hii inamaanisha kwamba zinahitajika kufanyika jitihada za makusudi katika kuhamasisha na kutangaza vivutio vya nyumbani ili kuwavutia watu wengi zaidi.   

Katika kulifanikisha hilo Jumia Travel imekuwa ikitoa punguzo kubwa la bei kila ifikapo siku ya Jumatano na kudumu mpaka siku ya Ijumaa kila wiki. Ofa hii hutoa fursa na kuwarahisishia watu wanaotamani kwenda kutalii sehemu fulani lakini wakihofia bei ya malazi kuwa juu.

Hoteli zote ambazo zimo kwenye orodha ya ofa hii zinapatikana kwenye maeneo ambayo yana vivutio vya kitalii kama vile mbuga za wanyama, milima, fukwe safi na za kuvutia za bahari, ndege wa kuvutia pamoja na vyakula na utamaduni wa eneo husika.  


PLANET BONGO - DAKIKA 10 ZA MAANGAMIZI NA FID Q


Kauli mpya ya Harmorapa baada ya kuitwa Nyani na Mose Iyobo

The DICOTA Chronicle January 2017 Issue: Bulding Our Future Together!!

$
0
0

Welcome to the DICOTA Chronicle Issue of January 2017.


Dear DICOTA Chronicle Readers!

At DICOTA exciting things are happening this year. To keep you and all our readers in the loop, the DICOTA chronicle issue for January 2017 contains a lot of information.  Please take some time to read it in its entirety. In the January 2017 issue "Building Our Future Together" is our binding message. DICOTA is excited to engage you and your community in the spirit of building stronger communities of the Tanzanian diaspora in America.
At the President's Corner, Mr. Charles Bishota’s message details the outlook for the organization going forward. The entire message from the president is shown below. In addition to the President's message, the DICOTA chronicle goes further to present in detail the DICOTA strategic plan for the next three years. To read the entire Newsletter click this link The Newsletter.


Building Our Future Together!
The President's Corner:
Let me begin by wishing you a prosperous 2017 marked with good health, humor, and inspiration. I commit as your president to embrace the vital responsibility of executing DICOTA’s mission. Each one of you is an integral part of our community and I vow to be candid in all my discourse.

Writing the President’s message is hallowing in the fact that it is not as simple as an Instagram or Facebook post. In social media, even when your musings do not make sense, people will humor your comments with a “like”. I pray you will humor my musings, as well.

Prior DICOTA presidents have immersed themselves in numerous beneficial works for the diaspora community. I am honored to follow in their footsteps. I am especially honored to follow in the footsteps of President Ndaga Mwakabuta. The task is daunting, however, together we will be stronger together.

DICOTA owes its structural health, as well as its gratitude, to the work of Dr. Ndaga. He purposely approached every undertaking and left our organization with a stronger foundation. There was neither an unfinished task, nor an unreturned phone call during his tenure. Thank you, Dr. Ndaga, for your outstanding leadership!

As you know, the DICOTA Executive Committee (“EC”) for 2017/18 consists of: Secretary General, Nisa Kibona, Deputy Secretary, Dr. Fundi Shaaban, Treasurer, Kwame Kinabo, Assistant Treasurer, Ana Matulile, EC at Large Members, Ms. Fatma Al-Tamim, and Dr. Frank Minja. This team is full of passion and deeply believes in DICOTA’s core mission.

In addition, Winston Churchill once said, “To improve is to change; to be perfect is to change often.” In preparation for this year, the EC team brings a new perspective as well as a creative commitment to all our initiatives. This crew is dedicated to serve. Our EC team will bring lasting change to our communities both here and at home. Please encourage them by dropping a note at dicota@dicotausa.org.

Furthermore, soon we will share with you many of our exciting activities (including our three-pronged strategic plan) in the next issue of The DICOTA Chronicle. The Tanzanian diaspora in America is rapidly changing and it’s becoming bigger. The tapestry of our society is as diverse as our adopted home. It includes (among others) our children in Texas, graduate students in Kansas, entrepreneurs in Maryland, professionals in California, and artists in Atlanta. The core of this community, is, its love and devotion for Tanzania.

Moreover, this year we have an opportunity to promote a spirit of unity. Please join in the ongoing national discourse regarding the Tanzanian diaspora and the national land policies. If you have not yet renewed your membership or registered as a new member, please click the following link to do so: register/renew your membership. While visiting the site, please register into our Diaspora Database. Registration to the Diaspora Database does not require active membership to DICOTA. Your registration benefits all Tanzanians in America by creating a central repository for networking.

Lastly, our next convention will be in Seattle, WA during the summer of 2018. Our brothers and sisters in Seattle are already working hard to prepare for your arrival. Stay tuned for more details.

Stronger Together,

Mr. Charles Bishota, Esq.
DICOTA President

NesiWangu: Free Trainings

$
0
0
Bofya: Free Trainings: Kwa maelezo zaidi piga simu443-808-1034 Kathleen Powell



WorkSource Montgomery is offering the following FREE trainings: CDL-B
Orientation February 8 at 1:30 PM
Apartment Maintenance
Starts February 27th 2017
Automotive Mechanics
Starts February 27th 2017
Space is Limited!! Sign up now


Spots are limited for eligible applicants only.

YOU ARE CORDIALLY INVITED.

$
0
0
The Montgomery County African Affairs Advisory Group cordially invites you to the launching of Mental Health Awareness Campaign. Mental Health Awareness is one of the top priorities on the agenda for the Montgomery County African Affairs Advisory Group (AAAG). Although Mental Health is a National focus, the African diaspora communities still experiences lack of awareness due to stigma, cultural barriers and beliefs. Moreover, Diaspora communities experience an overall lack of exposure and limited access to information on mental health as well as county resources that are readily available to them. Our goal is to ensure that, we are equipped with appropriate knowledge in providing intervention and accessing resources.


ALL WELCOME!.

1 Veterans Pl,
Silver Spring MD 20910
Date: February 9th, 2017
                                                               Time: 6:30 pm to 8:30 pm

FOR MORE INFORMATION CONTACT ;

County Liason: Daniel Koroma 301.523.6214
                                  Chair, Health Committee: Josphine Garnem 240. 666. 3375
Chair, AAAG Harriet Shangarai 240.6721788

Visit us at

MAGAZETI YA LEO FEBRUARY 01, 2017

PICHA: MAFURIKO YABOMOA NYUMBA, YAUA FAMILIA MPWAPWA

$
0
0
 Watu wanne wakiwamo watatu wa familia moja, wamefariki dunia baada ya nyumba zao kusombwa na mafuriko kutokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia jana katika Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.
Hata hivyo, viongozi mbalimbali wametoa takwimu zinazotofautiana kuhusu idadi ya vifo vilivyotokea.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alisema watu wanane walikuwa wameripotiwa kufariki dunia na kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ilikuwa inajiandaa kwenda eneo la tukio ili kujionea uharibifu uliotokea.
Lakini, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema taarifa alizonazo ni za watu watatu waliopoteza maisha na kwamba bado hajapata taarifa sahihi za tukio ambalo lilitokea katika vijiji vya Mang’angu na Chinyika katika Kata ya Ving’awe.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, mmoja wa manusura, Beka Mlami (10) alisema walikuwa wamelala wakiwa watano katika nyumba yao mvua kubwa ilipoanza kunyesha kuanzia saa tatu usiku na ilipofika usiku wa manane nyumba yao iliyojengwa kwa udongo ilisombwa na maji.
Mbali na yeye, wengine waliokuwa katika nyumba hiyo ni Martha Sumisumi (60), Shukuru Donald (15) aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Mwanakianga, Bernadetha Sumisumi (9) aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Ilolo na Joseph Sumisumi (12) ambaye alinusurika.
Beka alisema baada ya kuona maji yameingia ndani, aliwaambia ndugu zake wakimbie watoke nje na wakati wanajiandaa kuvaa nguo nyumba yao ilianguka na kuwaponda, lakini yeye alifanikiwa kutoka na kupanda juu ya bati.
Alisema baada ya kutoka nje ndipo gogo kubwa la mti lililosombwa na maji lilipopiga nyumba yao na kuanguka chini hivyo ndugu zake wengine kushindwa kutoka na hivyo kusombwa na maji.
Alisema baada ya kutoka nje alimwona ndugu yake mwingine Joseph akiwa anapelekwa na maji, lakini alifanikiwa kujiokoa.
 Mkazi mwingine wa eneo hilo, Steven Noel alisema nyumba iliyosombwa na maji ilikuwa imejengwa karibu na korongo la maji, hivyo baada ya mvua kunyesha, maji yaliacha mkondo wake na kuingia kwenye makazi ya watu na kusababisha maafa hayo.
“Mvua ilisababisha mafuriko makubwa ambayo yalikuwa yamebeba na magogo makubwa ambayo yaliipiga ile nyumba na kuivunja katikati,” alisema Noel.
Alisema baada ya gogo la mti kuipiga nyumba hiyo, maji yalijaa ndani na kwa kuwa milango ilikuwa imefungwa, yalikosa njia ya kutokea na kuiangusha.
Noel alisema kulipopambazuka, walifukua na kuipata miili ya watu hao watatu huku mwili mwingine wa Jesca Lubeleje (19) mkazi wa Kijiji cha Chinyika ukiokotwa.

SAKATA SHAMBA LA MBOWE SASA LAIBUA MENGINE

$
0
0
Hatua ya Serikali kumtaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kusitisha mradi wa kilimo cha kisasa kwa madai kuwa shamba lake liko kwenye chanzo cha maji imeibua hisia tofauti, ikihusishwa na nyingine zilizochukuliwa dhidi yake kwenye miradi mingine.
Kabla ya hatua hiyo, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, alipewa siku 14 kulipa kodi katika hoteli yake iliyoko jimboni humo na kabla ya hapo alihamishwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwenye jengo la Bilicanas, ikielezwa kuwa anadaiwa kodi ya pango wakati mwenyewe akisema alikuwa mmiliki mwenza.
Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gellasius Byakanwa amempa Mbowe miezi minne kuondoa mazao yote yaliyopo katika shamba hilo linalodaiwa kuwa ndani ya mita 60 karibu na Mto Weruweru, vinginevyo achukuliwe hatua za kisheria.
Wakili wa kujitegemea, Frank Robert aliitaka Serikali kusimamia sheria pasipo upendeleo wala ubaguzi ili jamii isitafsiri kama hatua inazozichukua zinalenga kudhibiti upinzani.
Alitolea mfano nyumba zaidi ya 160 zikiwamo za vigogo wa taasisi za umma na wastaafu katika mji wa Moshi ambazo zinadaiwa kujengwa ndani ya mita 60 katika mito ya Karanga na Rau.
Alisema anakumbuka Desemba 2015, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga alitangaza mpango wa Serikali kubomoa nyumba hizo lakini hakuna iliyobomolewa.
Hata hivyo, Wakili mwingine, Peter Mshikilwa alisisitiza kuwa ni makosa shughuli za maendeleo na kijamii kufanyika katika maeneo ya vyanzo vya maji na kwamba huo ni msimamo wa sheria kwa wote na si watu fulani tu.
Mbunge wa Moshi Vijijini (Chadema), Anthony Komu alidai anachofanyiwa Mbowe ni uhasama wa kisiasa zaidi kuliko kusimamia sheria na kutolea mfano wa nyumba hizo 160 za mjini Moshi.
Mbowe alipoulizwa na gazeti hili kuhusu sakata hilo, aliomba asizungumze chochote.

Nyumba 160
Februari 17 mwaka jana, Ofisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Seperatus Rutagenya alithibitishia gazeti hili kuanza kwa mchakato wa kubomoa nyumba hizo 160.
“Zoezi la kwanza lilikuwa ni kutambua watu walioingia ndani ya mita 60 na tumebaini nyumba zaidi ya 100 Mto Karanga na zaidi ya 60 kule Mto Rau,” alisema.
Alisema mchakati huo umeingia hatua ya pili ambayo ni kuwabaini kwa majina wamiliki wa nyumba hizo na kazi hiyo inatarajiwa kuwa limekamilika kufikia Febrauri 19.
Alisema pamoja na sheria kuwa wazi na Serikali kutangaza bomoabomoa, bado wapo watu ambao wameanza ujenzi upya ndani ya mita 60 na kuhoji wanapata wapi ujasiri huo.

Sakata la Bilicanas, hoteli
Uamuzi wa NHC kumwondoa Mbowe katika Jengo la Bilicanas, jijini Dar es Salaam na kutishia kufunga hoteli yake iliyopo Hai yamehusishwa na vita ya kisiasa ikidaiwa kwamba utekelezaji wake umemlenga Mbowe huku wengine wakiachwa.
Septemba Mosi mwaka jana, NHC ilitoa vifaa vyote vinavyotumiwa na Kampuni ya Free Media na kufungua vifaa vyote vya muziki kwenye klabu maarufu ya Bilicanas kwa madai kuwa anadaiwa pango zaidi ya Sh1.17 bilioni.
NHC pia ilitangaza wadaiwa wengine sugu ikisema wangechukuliwa hatua kama hiyo lakini hadi sasa hazijachukuliwa.
Alipotafutwa kwa simu jana, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu alipokea na baada ya kuulizwa kuhusu suala hili alisema yuko kikaoni, hivyo asingeweza kuzungumza. Baadaye aliomba atumiwe ujumbe mfupi lakini baada ya kutumiwa hakujibu.
Awali, Mchechu alisema Mbowe alikuwa ni miongoni mwa waliopewa notisi na hatua hiyo haina uhusiano wowote na masuala ya kisiasa.
Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Jaji mstaafu Amir Manento alisema asingependa kuzungumzia suala la Mbowe na NHC. Hata hivyo, alisema jambo la msingi haki lazima itolewe kwa wote.
“Naomba nizungumzie upande wa sheria inasemaje, kama sheria inawaruhusu NHC ni sahihi kumwondoa yeyote na katika masuala ya utekelezaji wa sheria huwezi kusema eti mbona fulani hajaondolewa. Pia, suala lao liliamuliwa na mahakama kwa hivyo kuna haki ilitendeka,” alisema Jaji Manento.
Mshauri wa masuala ya jinsia na mwanaharakati wa haki za binadamu, Gemma Akilimali alisema hatua zozote zinazochukuliwa na Serikali zinatakiwa kutekelezwa bila kuhusisha sura ya mtu. Alisema inapotokea kundi moja au upande fulani umeachwa inajenga wasiwasi kwenye jamii.
“Sisi tunaofuatilia tunapata wasiwasi kama zoezi lilikuwa ni genuine (halisi) au lilikuwa linalenga mtu mmoja tu, haitakiwi kuacha yeyote yule,” alisema.

CHANZO: MWANANCHI

WABUNGE WA UZAZI SALAMA WATAKA BAJETI YA AFYA YA UZAZI NA MTOTO KUBORESHWA

$
0
0
Mwenyekiti wa Kundi la Wabunge wa Uzazi Salama Mh. Jenista Mhagama (katikati) akifungua mkutano kati ya Muungano wa Utepe Mweupe (WRATZ) na Wabunge wa uzazi salama. Meneja Mradi wa Muungano wa Utepe Mweupe (WRATZ), Bi. Sizarina Hamisi (mbele) akiwasilisha mada katika mkutano kati ya WRATZ na kundi la Wabunge wa uzazi salama mjini Dodoma.
Mkutano kati ya Muungano wa Utepe Mweupe (WRATZ) na Wabunge wa uzazi salama ukiendelea.
WABUNGE wa kundi la uzazi salama wametakiwa kuhamasisha na kutetea Bajeti ya Afya ya Uzazi na Mtoto ili ipewe kipaumbele katika mipango ya Halmashauri kwa mwaka 2017/2018. Hamasa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kundi la Wabunge wa Uzazi Salama, Mh. Jenista Mhagama wakati akifungua mkutano uliowakutanisha wabunge wa kundi hilo wapatao 30 pamoja na Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama (WRATZ) mjini Dodoma kujadili kuhusu mchango wa wabunge katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Akiwasilisha mada katika mkutano huo Meneja mradi wa Muungano wa Utepe mweupe (WRATZ) Bi Sizarina Hamisi alisema kwa mujibu wa takwimu ya Idadi ya Watu na Afya Tanzania ya mwaka 2015-2016 zinaonyesha kuwa kwa sasa wakina mama 30 na watoto wachanga 180 wanapoteza maisha kila siku kutokana na matatizo yatokanayo na uzazi.
 Kwa upande wao baadhi ya wabunge wamekiri kuwa pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali bado vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi ni changamoto hivyo kuna haja yakuongeza jitihada ili kutatua tatizo hilo ikiwemo bajeti ya afya ya mama na mtoto hasa huduma za muhimu na dharura kupewa kipaumbele kuanzia ngazi za halmashauri mpaka serikali kuu.

MGODI WA BUZWAGI WAZINDUA KAMPENI YA WAKIA MOJA MTI MMOJA,MITI MILIONI 1.6 KUPANDWA KAHAMA

$
0
0


Mkuu wa wilaya Kahama Fadhili Nkurlu akipanda mti kuashiria uzinduzi rasmi wa kampeni ya upandaji miti milioni moja na laki sita itakayopandwa katika maeneneo mbalimbali wilayani kahama kwa lengo la kutunza mazingira pamoja na kuufanya mji wa Kahama upendeze.

Mkuu wa wilaya kahama Fadhili Nkurlu akimwagia maji mti alioupanda wakati alipozindua kampeni ya upandaji miti
Mkuu wa polisi wilaya ya Kahama Mussa Mchenya akishiriki pia upandaji miti.
Afisa Usalama wa Wilaya ya Kahama Aretus Lyimo akishiriki upandaji miti wakati wa zoezi la uzindunzi wa upandaji miti milioni moja na laki sita.
Katibu Tawala wa Wilaya Kahama Timothy Ndanya akishiriki pia kupanda miti.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo akifurahia wakati alipokuwa akipanda mti katika eneo la mgodi wa Buzwagi.
Meneja raslimali watu wa Mgodi wa Buzwagi Solomon Rwangabwoba akifurahia kupanda mti wakati wa uzindunzi wa kampeni ya upandaji miti milioni moja na laki sita itakayoendeshwa na mgodi wa Buzwagi.
Afisa Mkuu Mwendeshaji wa Kampuni ya Acacia Mark Marcombe akishiriki zoezi la upandaji miti milioni moja na laki sita miti ambayo inatajwa kuwa itasaidia katika kuipendezesha wilaya ya Kahama.
Afisa Mkuu wa Idara ya Raslimali watu wa Kampuni ya Acacia Peter Gereta akishiriki zoezi la upandaji miti.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Acacia anaeshughulikia Masuala ya Kampuni (Corporate Affairs) Deo Mwanyika akishiriki pia kupata mti.
Mh. Salome Makamba MB-(Viti Maalumu) akishiriki pia upandaji miti baada ya kupita karibu na eneo ambapo zoezi la upandaji miti lilikuwa likifanyika na akaona ni vyema na yeye akashiri katika kuunga mkono jitihada za Mgodi wa Buzwagi katika kupanda miti itakayosaidia katika utunzaji wa mazingira wa wilaya ya Kahama na Taifa kwa ujumla.
Afisa Mkuu wa Idara ya Utafiti wa madini (Exploration) Peter Spora akifurahia wakati alipokuwa akipanda mti katika eneo la Mgodi wa Buzwagi.




Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi leo umezindua kampeni ya upandaji miti katika Wilaya ya Kahama ikiwa na lengo la kupanda mti kwa kila wakia ya dhahabu ambayo imechimbwa kwenye mgodi wa Buzwagi, ambapo miti zaidi ya milioni moja na laki sita inatarajiwa kupandwa katika kipindi cha miaka miwili.
Akizindua kampeni hiyo Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu ameupongeza uongozi wa Mgodi wa Buzwagi kwa hatua hiyo na kusema ni ya kizalendo kwa kuwa itasaidia katika kuboresha hali ya mazingira ya wilaya ya Kahama.
“Jukumu la upandaji miti na kuhakikisha mazingira yetu yanatunzwa ni letu sote, Wenzetu wa Buzwagi wameanza kuonyesha jitihada kwa kupanda miti milioni moja na laki sita, hivyo sote kama Jamii hatuna budi kuwaunga mkono kwa kuhakikisha kila mmoja wetu katika eneo lake anapanda miti na kuifanya wilaya yetu ya Kahama izidi kupendeza”Alisema Nkurlu.
Akizungumzia Malengo ya Kampeni hiyo Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo amesema kama wadau muhimu wa mazingira wanalojukumu la moja kwa moja kuhakikisha shughuli za utunzaji wa mazingira zinakuwa ni sehemu ya maisha ya kila siku.
Na kupitia mipango ya muda mrefu uongozi umejiwekea lengo la kupanda mti mmoja kwa kila wakia moja ya dhahabu itakayokuwa ikizalishwa katika kipindi chote cha uhai wa Mgodi wa Buzwagi ambapo inakisiwa mpaka shughuli za uzalishaji zitakapositishwa takribani wakia milioni moja na laki sita zitakuwa zimezalishwa.
“Leo tunazindua awamu ya kwanza ya kampeni hii ambayo itahusisha upandaji wa miti laki tano, ambapo mpaka sasa miti elfu ishirini imekwisha pandwa na tunatarajia mpaka mwisho wa mwaka huu awamu ya kwanza ya miti laki tano itakuwa imepandwa” Alisema Mwaipopo. “
“Kwa kupanda miti hii, tunakusudia kuwa sehemu muhimu ya wadau wa mazingira wenye lengo la kuipendezesha wilaya yetu ya Kahama, pia kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na kuonyesha utayari wetu kama Kampuni katika kurejesha katika hali ya awali ya mazingira ya eneo la Mgodi itakapofikia wakati wa kuufunga. Aliongeza Mwaipopo.
Miti aina mbalimbali inatarajiwa kupandwa katika zoezi hili huku mti maarufu wa “Acacia” unaobeba jina la Kampuni mama ya Acacia Mining Plc inayomiliki Mgodi wa Buzwagi ikiwa ni sehemu ya miti itakayopandwa,
Huku zaidi ya shilingi milioni mia sita na arobaini na tano zikitarajiwa kutumika katika awamu ya kwanza ya upandaji miti laki tano.
Katika hatua nyingine maafisa wakuu wa Kampuni ya Acacia kutoka ofisi za Acacia Mining Plc London pamoja na Dar es salaam walishiriki pia katika zoezi la upandaji miti katika eneo la Mgodi wa Buzwagi wakati walipofanya ziara ya kikazi mgodini hapo.
“Wakia Moja Mti Mmoja”
Imetolewa na Idara ya Mawasiliano Mgodi wa Buzwagi
Simu  +255 22 2164 200

Hii ndio ratiba ya raundi ya tano ya kombe la FA

$
0
0
Ratiba ya raundi ya tano ya kombe la FA imetoka huku bahati kubwa wakionekana kuipata timu ya Sutton United ambayo imepangiwa kucheza na Arsenal. Sutton hiyo ndio itakuwa mechi yao kubwa zaidi kuicheza katika historia ya timu hiyo.

Hii ndio ratiba kamili ya FA Cup.

Burnley v Lincoln City
Fulham v Tottenham
Blackburn Rovers v Manchester United
Sutton United v Arsenal
Middlesbrough v Oxford United
Wolves v Chelsea
Huddersfield v Manchester City
Millwall v Derby County or Leicester City

Mechi hizo zitachezwa February 17 na February 20.

IBADA YA KISWAHILI FEB 5, 2017

IZARA YA MALIASILI NA UTALII YAWAPIGA MSASA WABUNGE WA KAMATI YA KUDUMU YA ARDHI,MALIASILI NA UTALII KUHUSU CHANGAMOTO ZA UHIFADHI WA WANYAMAPORI NCHINI

$
0
0
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) David Kanyatta akiwasilisha mada kwa Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu madhara ya kulishia mifugo ndani ya hifadhi kunavyoathiri sekta ya utalii katika semina iliyofanyika jana mjini Dodoma ( Picha na Lusungu Helela- Maliasili)
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Yussuf Hussein, akichangia hoja mara baada ya mada kuweza kuwasilishwa na wataalamu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu utalii wa baharini ambao umekuwa haupewi kipaumbele katika kutangazwa pamoja na kuendelezwa katika semina hiyo
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Marwa Chacha, (katikati) akichangia hoja mara baada ya mada kuweza kuwasilishwa na wataalamu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu wanyamapori waharibifu wa mazao kama vile tembo wanavyoathiri maisha ya wapiga kura wake kwenye vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti katika semina iliyofanyika jana mjini Dodoma. Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Atashasta Nditiye, (katikati) Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe ( kushoto) pamoja na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani ( wa kwanza kulia) wakifuatilia kwa makini michango ya wajumbe wa kamati hiyo wakati walipokuwa wkichangia hoja kuhusu mada mbalimbali zilizotolewa na wataalamu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu madhara ya kulishia mifugo ndani ya hifadhi, tatizo la ujangili wa tembo na faru pamoja madhara yanayosababishwa na wanyama waharibifu wa mazao kama vile tembo katika vijiji vinavyozunguka hifadhi nchini, iliyofanyika jana mjini Dodoma
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Devota Minja, MB ( wa kwanza kulia) pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalamu wa Wizara hiyo kuhusu madhara ya kulishia mifugo ndani ya hifadhi, tatizo la ujangili wa tembo na faru pamoja madhara yanayosababishwa na wanyama waharibifu wa mazao kama vile tembo katika vijiji vinavyozunguka hifadhi nchini katika semina iliyofanyika jana mjini Dodoma. Kwa upande wa kushoto ni viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj.Gen. Gaudence Milanzi ( wa kwanza kulia) pamoja na na viongozi wa taasisi katika semina ya kamati ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii iliyofanyika jana mjini Dodoma
Viewing all 45921 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>