Quantcast
Channel: VIJIMAMBO
Viewing all 45987 articles
Browse latest View live

SAIDA KAROLI "MARIA SALOME" JIKUMBUSHE NA HII KIPINDI HICHO ULIKUWA WAPI


Marudio ya kipindi cha MISHUMAA YA KALE.....Ijumaa Januari 30, 2015

$
0
0
Kama ilikosa kipindi cha MISHUMAA YA KALE leo (Ijumaa Januari 30, 2015), karibu.
Kwanza ka-kideo
 
Kisha.... Kipindi kamili

Mh.Mbatia: Jeshi la polisi lifanyiwe marekebisho ya kimfumo ili kuboresha utendaji wake

$
0
0
Serikali imeshauriwa jeshi la polisi lifanyiwe marekebisho ya kimfumo ili kuboresha utendaji wake ambao kwa sasa unalalamikiwa kwa sehemu kubwa na wananchi kwa kukiuka haki za binadamu.
Akizungumza jana mjini Dodoma katika kuhitimisha hoja kuhusu kukamatwa kwa kiongozi wa wa chama cha CUF, Prof Ibrahim Lipumba na wanachama wake,Mbatia alisema kuwa kitendo hicho kilikiuka haki za binadamu ikiwemo wanawake kudhalilishwa kijinsia.

Mh. Mbatia emeongeza kuwa ili chaguzi zijazo ziwe za amani na utulivu ameishauri serikali kubadilisha sera za vyama vya siasa na utawala pamoja na mfumo wa jeshi la polisi kuendeleza amani na utulivu ambavyo kwa sasa vinaonekana kuanza kutoweka.

Ukweli Kuhusu Tevez Aliyekatwa Uume Wake Baada ya Kuwazulumu Madawa ya Kulevya Wenzake

$
0
0
HABARI ZA UHAKIKA JUU YA SAKATA LA JUMAANNE TEVEZ. Nikweli kwamba huyu bwana yuko South Africa Pretoria. Bwana Tevez alodhaminiwa mzigo na vijana wenzake huko Bondeni kwamba akauze kisha alete Mpunga. Mdhamini alikuwa ni Kijana wa Kibongo anayeonekana pichani anayeitwa Jeff Katili mtoto wa Ilala ambaye maskani yake ni South. TEVEZ baada ya kuchukua mzigo uliokuwa na thamani ya takriban milioni mia moja na hamsini (150,000,000/=) aliingia mitini hakurudi tena. Kilichotokea Jeff baada ya kubanwa na wana akawaambia kuwa tulieni nitamleta tu.
Basi Jeff akamrubuni Tevez kuwa njoo Kuna kazi.. Tevez akaingia mzima mzima akaenda hadi Pretoria wiki iliyopita na kufikia kwa Jeff Katili na kupata mapokezi mazuri kama kawaida. Baada ya kufika walitoka kwenda matembezi KWAZULU NATAL... wakiwa huko walifikia kwa washkaji zao wa kibongo lakini kwenye nyumba ambayo ilikuwa kama holi haina chochote ndani. Chini lilitandikwa karatasi la nailoni ili kuepusha damu isitapakae. Alibanwa juu ya mzigo na mtesaji mkubwa alikuwa Jeff Katili mwenyewe ambaye ni mdhamini. Tevez hajang'olewa jicho bali alipigwa Ngumi hadi jicho likaenda ndani... NGUMI YA MTOTO WA KIUME.

Ameteswa sana na amekatwakatwa na viwembe mwili mzima. Zakari yake haijakatwa kama picha zilivyoonyesha bali imekatwa na viwembe. Taarifa zilitumwa kwa kaka yake na akina Jeff na kuwataka watume pesa la sivyo wanamuua. familia kupitia kaka yake imeshatuma pesa nusu na sas anatibiwa hukohuko South na atarejea punde. Uzushi kuwa amekufa hauna ukweli na hizi ni habari kamili kutoka kwa watu wa karibu na familia hiyo.

LIGI DARAJA LA KWANZA TANZANIA BARA KUNDI A

Michigan & Ohio : We Are Picking Up This February 7th

AMCHINJA MPENZI WAKE MPAKA KUFA KISA WIVU WA MAPENZI

$
0
0
Kijana anaetuhumiwa kumchinja mpenzi wake sababu ya wivu wa mapenzi akiwa amepandishwa katika gari la Polisi akipelekwa kituoni huku akitokwa na damu shingoni baada ya kujaribu kujiua kwa kutumia kisu
Mwili wa Msichana anaedaiwa kuchinjwa na mpenzi wake leo jioni maeneo ya Manzese Friends Corner ukitolewa katika eneo la tukio

Tanga kuwa na timu tatu Ligi Kuu ijayo?

$
0
0
Kikosi cha Costal Union ya Tanga 

Timu za Tanga zilizopo Ligi Kuu kwa sasa ni Coastal Union na Mgambo JKT.
IWAPO African Sports itafanikiwa kupanda Ligi Kuu Bara, basi Mkoa wa Tanga utakuwa na timu tatu kwenye ligi hiyo msimu ujao.
Timu za Tanga zilizopo Ligi Kuu kwa sasa ni Coastal Union na Mgambo JKT.
African Sport inaongoza Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza ikiwa imecheza michezo 19 huku ikibakiza mitatu kufunga hesabu.
Kanuni za Ligi hiyo zinasema kuwa timu mbili zitakazomaliza ligi hiyo kwenye nafasi za juu kwenye kila kundi, zitapanda Ligi Kuu na hali ilivyo African Sports wamejiweka pazuri kwani wanahitaji pointi nne pekee.
Kama timu hiyo itashinda mchezo mmoja na kutoa sare mmoja tu itafikisha pointi 45 na tayari itakuwa imefuzu kushiriki Ligi Kuu kwani hakutakuwa na timu nyingine ambayo itaweza kupita pointi hizo.
Katika hatua nyingine, mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu 2014/15 unakaribia tamati na mpaka sasa Coastal Union ipo kwenye nafasi ya tano ikiwa kwenye pointi 16 wakati Mgambo wako kwenye nafasi ya tisa ikiwa na pointi 14.
Hali hii inaashiria kuwa iwapo timu hizo zitaendelea kubaki basi uhasimu wa Coastal na African Sports kwenye soka utafufuka.
Source:Mwanaspoti

NG'ARI NG'ARI S3E01 - D ( By SAKINA LYOKA ).mp4

UNYAMA, UDHALILISHWAJI MTALAKA WA ISHA MASHAUZI UKWELI NI HUU

$
0
0
Mfanyabiashara, Jumanne Hassan ‘Tevez’ akiwa amefungwa kamba na watesi wake.
Stori: Musa Mateja GPL/Risasi

HATIMAYE ukweli wa kutekwa, kuteswa kwa kudhalilishwa kwa aliyekuwa mume wa mwimba taarab mahiri Bongo, Aisha Ramadhan ‘Isha Mashauzi’, Jumanne Hassan ‘Tevez’, umejulikana, Risasi Jumamosi limechimba.
Januari 28, mwaka huu, picha za Tevez akiwa ametoka kuteswa kwa kudhalilishwa zilisambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii huku wengine wakidai kisa ni kukutwa na mke wa mtu, wengine wakisema ni dhuluma.

RISASI LAINGIA MTAANI KUCHIMBA
Risasi Jumamosi halikufanya haraka kuichapisha habari hiyo mpaka kuichimba kwanza ili kujua kisa na mkasa kamili ndipo iwapelekee wasomaji wake. Na ndivyo ilivyofanyika!

ENEO LA TUKIO
Risasi Jumamosi lilichimba na kubaini kuwa, tukio la Tevez kufanyiwa ukatili huo lilitokea kwenye mji wa Durban nchini Afrika Kusini ambako alikwenda kibiashara.
“Tukio si la Dar kama wanavyosema wengine, limetokea mjini Durban, Afrika Kusini. Si unajua jamaa (Tevez) ni mtu wa tripu za kibiashara!” alisema mtoa habari mmoja akiomba hifadhi ya jina lake.

Jeraha likiwa mgongoni mwa Jumanne Hassan ‘Tevez’ baada ya kuteswa.

WALIOFANYA UKATILI
Kwa mujibu wa chanzo hicho, watu waliomtenda Tevez ni jamaa zake anaofanya nao biashara ambayo Risasi Jumamosi halijaijua vizuri (ingawa kwenye mitandao ya kijamii wanadai ni madawa ya kulevya).

YATAJWA DHULUMA
Chanzo kikaanza kuanika historia nzima tangu Tevez hajafanyiwa utekaji na udhalilishwaji huo.
“Siku za nyuma Tevez alipewa mzigo nchini Tanzania ili awapelekee hao jamaa wa Afrika Kusini. Aliondoka jijini Dar kwenda Nairobi, Kenya kwa basi akiwa na begi.
“Alipofika Nairobi, ilidaiwa begi hilo alilisahau kwenye basi lakini wengine wanasema aliuuza Nairobi na kwenda Afrika Kusini akiwa na begi feki.”

TEVEZ AWASILI AFRIKA KUSINI, AKUMBANA NA MSALA
Habari zaidi zikachimbuka na kudai kwamba, Tevez aliwasili mjini Durban na kukutana na jamaa zake ambapo aliwaambia mzigo aliusahau kwenye basi.
“Kumbe inasemekana jamaa aliyemuuzia mzigo Nairobi anafahamiana na jamaa wa Sauz na aliwapigia simu kuwaambia kwamba, ameuziwa mzigo na Tevez.
“Kwa hiyo mpaka Tevez anawasili kule, jamaa walikuwa wanajua hana mzigo kwa kuwa aliuuza Nairobi,” kilisema chanzo.

‘Tevez’ akiwa na moja ya wadau wenzake katika biashara anazofanya huko Durban. 


ATEKWA, ADHALILISHWA
Ikaendelea kudaiwa kuwa, madai ya Tevez yaliwakera jamaa kwa vile walijua kila kitu, hivyo walimteka na kuanza kumtesa kwa kumvua nguo zote, wakamfunga kamba za manila za rangi ya bluu na kuanza kumtesa kwa adhabu mbalimbali ili kumkomesha.
Inadaiwa katika adhabu hiyo, jamaa hao walimpiga na kitu chenye ncha kali hali iliyosababisha Tevez atokwe na damu na ngozi kuchubuka eneo la mgongoni.

MADAI WAKATI WA UDHALILISHWAJI
Inadaiwa wakati udhalilishaji huo ukiendelea, jamaa hao walikuwa wakisema wanachotaka ni mzigo wao na si kitu kingine.

MARAFIKI, JAMAA WA DAR
Kufuatia kusambaa kwa picha hizo mtandaoni, marafiki na jamaa wa Tevez waliopo Bongo walilazimika kufanya mpango kwa kuwasiliana na watu wa karibu waliopo Durban kumnusuru Tevez kwa kumpeleka hospitali ambako anapata matibabu hadi juzi, Alhamisi.
Risasi Jumamosi: “Kuna habari alikatwa sehemu za siri ni kweli?”
Chanzo: “Si kweli.”

Risasi Jumamosi: “Inasemekana alifanyiwa kitu mbaya cha mambo ya Sodama, ni kweli?”
“Si kweli. Watu wanasema tu. Ila walimtesa sana kwa kweli.”

Bw. Jumanne Hassan ‘Tevez’ akiwa na moja ya jamaa zake sauzi.

RISASI LATINGA DUKANI KWA MKEWE WA SASA
Ili kuzidi kupata habari zaidi, Januari 28, mwaka huu, usiku Risasi Jumamosi lilikwenda Kinondoni Kwamanyanya, Dar kwenye duka la mke wa sasa wa Tevez ili kumsikia anasema nini kuhusu tukio hilo.
Paparazi wetu hakumkuta mke huyo lakini alibahatika kuongea na msichana aliyekuwa nje ya duka hilo na kumuuliza aliko Tevez.

Msichana: “Tevez yupo safarini Morogoro.”
Risasi Jumamosi: “Mbona hapatikani hewani? Nipe namba zake nyingine.”
Msichana: “Nilizonazo ndiyo hizohizo ulizonazo wewe, ni…(akazitaja).”
Kweli namba hizo ndiyo alizokuwa nazo paparazi wetu.

MAMA MKWE WA TEVEZ
Kesho yake, Risasi Jumamosi lilimsaka kwa simu mama mkwe wa zamani wa Tevez (mama wa Isha) lengo ni lilelile, kutaka kujua kama naye ana taarifa hizo na anasemaje.
“Ni kweli nimesikia na nimeona picha zake yaani nimesikitika sana kiasi kwamba nikawa siamini kama ni kweli yeye anaweza kufanyiwa ukatili wa aina hiyo.

“Kikubwa namshukuru Mungu kusikia yupo hai na kwa maana hiyo namuombea zaidi ili arudi katika afya yake,” alisema mama mkwe huyo aitwaye Rukia Juma.

Bw. Jumanne Hassan ‘Tevez’akiwa na mkewe.

MTU WA KARIBU NA TEVEZ
Risasi Jumamosi liliendelea kutafuta undani zaidi wa tukio la Tevez kwa kuongea na watu wake wa karibu waliopo Durban, ndipo likapenyezewa ishu mpya kuwa, baadhi ya ndugu na wafanyabiashara wenzake na Tevez wamechanga na kurudisha mali zilizokuwa zikidaiwa na jamaa hao.
“Nilikuwa Durban muda si mrefu na hapa ndiyo narejea nyumbani (Bongo). Kiukweli tukio la Tevez ndiyo habari ya mjini Sauz, maana jamaa wamemfanyia mbaya kinoma lakini kusema kweli hajakatwa nyeti kama mitandao ya kijamii inavyoandika, wamempiga sana.”
“Kingine ambacho ninajua tayari ameshatolewa kwenye jengo alilokuwa ametekewa na sasa yupo hospitali maalum ambayo siwezi kukutajia, ila huenda hali yake ikawa nzuri kama kweli atakuwa chini ya uangalizi wa madaktari,” alisema jamaa huyo.
Source:GPL

DIAMOND ALICHOKISEMA KUHUSU EX WA ZARI

$
0
0

Stori: Musa Mateja/Risasi
ICON wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati aliamua kumtolea uvivu, aliyewahi kuwa mpenzi wa mwandani wake wa sasa, Zarinah Hassani ‘Zari’, King lawrenc kwa kumuita mpuuzi anayetafuta kiki kwa vile kila kukicha kazi yake ni kumfuatafuata kwa maneno ya kejeli na kumtusi.

X wa Zari, King lawrence akipozi.

Akipiga stori mbili tatu na gazeti hili hivi karibuni, staa huyo alisema mara nyingi amejitahidi kumpuuza kwa kitendo chake cha kumkejeli katika mitandao ya kijamii, lakini kitu alichogundua ni kwamba mpenzi huyo wa zamani wa Zari anataka yeye amjibu ili aweze kulikuza jina lake, kitu ambacho ni cha kijinga.
Zarinah Hassani ‘Zari’.
“Nimejitahidi sana kukaa kimya kila anaponitusi huyu jamaa, lakini kumbuka mimi ni binadamu, najaribu kuliangalia jambo hili nagundua kwamba hana chochote cha msingi anachoongea zaidi ya matusi, anatafuta nimjibu kitu ili apate kiki aweze kutimiza ndoto zake,” alisema Diamond na kuongeza:
ICON wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na Zari.
“Nashukuru nimegundua hana mada ya kuzungumza katika mitandao zaidi ya mimi na Zari, ningemshauri aendelee na shughuli zake za kila siku, asihangaike na kitu asichokijua, kugombana na mimi ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa, mimi nawaza nifanyeje ili niweze kuitangaza nchi yangu, yeye anawaza afanyeje ili aweze kupandisha jina lake, siwezi kubishana na mpuuzi.”

Mwanaume huyo Mganda, kwa muda mwingi amekuwa akiweka picha zake, Zari na Diamond akisindikiza na maneno ya kejeli na dhihaka dhidi ya mkali huyo wa Bongo Fleva, katika kile kinachoonekana kuwa ni kushikwa na wivu.

WIMBO WANGU WA LEO

Karibuni wote Jumapili hii ya Februari 1, 2015 – Ibada Itaanza Saa kumi kamili 4:00EST

$
0
0
Bwana Asifiwe!
Karibuni wote Jumapili hii ya Februari 1, 2015 tumwabudu
Mungu wetu na kusikiliza neno lake kwa lugha yetu ya Kiswahili.
Kwa wale washabiki wa "Super Bowl" karibu sana, muda utazingatiwa. Mbarikiwe!

MEYA MANISPAA MOROGORO, WAANDISHI WA HABARI WAPATA AJALI

$
0
0
Wasamalia wakimuwahisha Hospital,Mmoja wa majeruhi mara baada ya kupata ajali eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .
Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Rajab Rutengwe ( wa kwanza kushoto) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro , Said Amanzi , wakipita eneo ambalo gari la namba SM 4151 Nissan iliyokuwa ikitumiwa na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo , ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani -Msamvu barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .Meya huyo na watu wengine watatu walijeruhiwa na kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na kulazwa wakindelea kupatiwa matibabu.
Gari la Meya likiwa halitamaniki.
Hili ndilo basi lililogongana na Gari ya Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.
Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo ,(45) akiwa amelazwa wodi namba tano ya daraja la kwanza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya kujeruhiwa kufuatia gari yake SM 4151 ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani , Msamvu Barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam ,mbali na Meya huyo na watu wengine watatu ,Dereva Mwambala Ally (55), na waandishi wa habari , Anita Chali (30) pamoja na HUSSEIN Nuha (28) pia walijeruhiwa na kulazwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya kupatiwa matibabu. ( Picha na John Nditi).
Mwandishi wa habari,Anita Chali akiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya kujeruhiwa kufuatia gari waliyoipata,walipokuwa kwenye kazi na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Rajab Rutengwe akionesha eneo ambalo gari la namba SM 4151 Nissan iliyokuwa ikitumiwa na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo , ilipogongwa Januari 30, mwaka huu saa 9: 30 alasiri eneo la Mzambarauni Darajani , Msamvu Barabara kuu ya Moro- Dar na Basi la Abiria aina ya Scania yenye namba za usajili T 831 CEH (Happy Africa ),iliyokuwa ikitokea mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam .Meya huyo na watu wengine watatu walijeruhiwa na kupimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro na kulazwa wakindelea kupatiwa matibabu.


Na John Nditi ,Morogoro


MEYA wa Halmashauri ya Manispaa Morogoro , Amir Nondo (45), dereva na waandishi wa habari wawili wamepata ajali baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongwa na basi la abiria lenye namba za usajili T 831 CEH, aina ya Scania mali ya kampuni ya Happy Africa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao na kulazwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.


Tukio hilo lilitokea Januari 30, mwaka huu majira ya saa 9: 30 alasiri , eneo la Msamvu Mzambarauni darajani katika barabara kuu ya Morogoro- Dar es Salaam, ambapo basi hilo lilikuwa likotokea mkoani Njombe.


Majina ya watu hao wengine waliojeruhiwa na kulaza katika wodi za daraja la kwanza katika hospitali ya rufaa ya mkoa , ni dereva wa gari la Meya, Mwambala Ally (55) , na waandishi wa habari ambao ni wapigapicha vituo vya televisheni , Anitha Chali (30) pamoja na Hussein Nuha (28).


Mstahiki meya huyo aliyekuwa kwenye gari ya Halmashauri ya Manispaa hiyo yenye namba za usajili SM 4151, ikiendeshwa na Mwambala ambamo pia walikuwemo waandishi wa habari hayo na alikuwa katika msafara wa ziara ya kikazi ya mkuu wa mkoa huo,Dk Rajab Rutengwe.


Meya Nondo akizungumzia ajali hiyo, akiwa wodini akipatiwa matibabu ,sambamba na majeruhi wengine alisema baada ya kufika eneo la Mizambarauni, Darajani, lilichomoka pembeni basi la abiria ililokuwa likitokea Njombe kuelekea Dar es salaam, na kuligonga kwa mbele gari alilokuwemo.


Mashuhuda wa ajali hiyo waliwaambia waandishi wa habari wakiwa eneo la tukio, kuwa chanzo cha ajali hiyo ni basi la abiria mali ya kampuni ya Happy Africa, kuingilia msafara huo wa mkuu wa mkoa uliokuwa ukielea mjini baada ya kukagua shughuli za ujenzi wa vyumba vya maabara na kuzungumza na wananchi wa Kata ya Bigwa katika Shule ya Sekondari Sumaye.


Mkuu wa mkoa kwa takribani wiki mbili amekuwa katika ziara katik halmashauri saba za mkoa huo kwa ajili ya kukagua shughuli za ujenzi na umaliziaji wa maabara tatu kwa kila shule ya skondari ya Kata na pia kutumia fursa hiyo kujitambulisha , kusikiliza kero na kuzipatia majawabu ya msingi.


Januari 29 na 30 mwaka huu ilikuwa ni zamu ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Shule ya sekondari Sumaye kilikuwa ni kituo chake cha mwisho katika ziara hiyo na baadaye kufanyika kwa majumuisho ya ziara hiyo Januari 31, mwaka huu mjini Morogoro.


Hata hivyo baada ya kufikishwa hospitali ya rufaa ya mkoa , viongozi mbalimbali walifika kuwajulia hali wakati wakiendelea kupatia matubabu na madaktari mbingwa wa hospitali hiyo, akiwemo Mganga mkuu wa mkoa , Godfrey Mtei.


Mstahiki Meya Nondo ameumia sehemu ya kichani na mkononi , wakati na mpiga picha Anita Chali, ameumia kichwani, huku dereva pamoja na Hussein wakiumia zaidi kwenye paji la uso na kichwani huku Hussein akisaidiwa na mashine ya kupumulia (oxygen).


Kufuatia tukio hilo Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa mkoa imesema itatoa taarifa ya ajali hiyo jumamosi ya Januari 31, mwaka huu

CHIPUKIZI WA UVCCM WAJIFUA VIKALI TAYARI KWA KILELE CHA MIAKA 38 YA CCM KESHO, SONGEA

$
0
0
Chipukizu hao wakiwa kwenye mazoezi ya halaiki
Mshika bendera ya CCM kwenye kikosi cha Bendera cha Gwaride la Umoja wa Vijana wa CCM, Sharif Mohammed na wenzake wakipita kwa ukakamavu mbele ya jukwaa kuu wakati wa mazoezi ya mwisho ya gwaride na halaiki kwa ajili ya Kilala cha Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM yanayofanyika kesho Kitaifa kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea mkoani Ruvuma 
Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Vijana wa Chipukizi wa CCM wakionyesha mazoezi ya ukakamavu wakati wa mazoezi yao ya mwisho leo kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Vijana wa Chipukizi wakionyesha ohodari wao wa mazoezi ya 'kikomandoo' wakati wa mazoezi yao ya mwisho ya paredi na halaiki kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya miaka 38 ya CCM kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea
Mmoja wa Chipukizi wa CCM waliokuwa katika mazoezi hayo akisaidiwa baada ya kuanguka kutokana na mazoezi hayo ya mwisho kupamba moto. Alipata ahueni baada ya kupatiwa huduma ya kwanza.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Mratibu wa Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM, Emmanuel Nchimbi, walipokuwa wakikagua mazoezi ya vijana wa Chipukizi wa CCM ya paredi na halaiki kwa ajili ya Maadhimisho ya Kilele cha Miaka 38 ya CCM, yatakayofanyika Kitaifa kesho kwenye Uwanja wa majiMaji mjini Songea.
Vijana wa Chipukizi wa CCM waliopo katika mazoezi ya halaiki na paredi kwa ajili ya Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM mjini Songea, wakikipiga saluti wakati wa mazoezi ya mwisho leo kwenye uwanja wa Majimaji
Kijana wa Chipukizi wa CCM Mbaraka Ngonyani akionyesha umakini wake wakati akipiga saluti wakati wa mazoezi hayo ya mwisho leo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa UVCCM Sixtus Mapunda wakitazama mazoezi ya mwisho ya Chipukizi hao. Picha zote na Bashir Nkoromo

BALOZI IDDI AFUNGUA MKUTANO WA 18 WA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

$
0
0
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Pandu Ameir Kificho akiambatana na Makatibu na walinzi wa Baraza hilo wakitoa nje mara baada ya kufungwa kwa Mkutano wa 18 wa Baraza la Wawakilishi Mbweni.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifunga Mkutano wa 18 wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliokuwa ukiendelea katika ukumbi wa Majengo ya Baraza hilo uliyopo Mbweni Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Aliyepo meza ya juu ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho. Picha na – OMPR – ZNZ.
*************************************************
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakamilisha utafiti wa kuibua vivutio vipya vya Utalii vilivyopo katika maeneo ya vijiji nchini ambapo matokeo ya utafiti huo yatasambazwa kwa wanachi ili kuongeza uelewa wa fursa za sekta ya utalii zilizomo katika maeneo yao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati akiufunga Mkutano wa 18 wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar uliokuwa ukiendelea katika ukumbi wa Majengo ya Baraza hilo yaliyopo Mbweni Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Balozi Seif alisema utekelezaji wa mpango huo unatarajiwa kutoa ajira za moja kwa moja zaidi kwa Wananchi hasa wale wa Vijijini katika kuendeleza ile azma ya Serikali ya kuimarisha Utalii kwa wote.
Alisema mwishoni mwa mwaka uliopita Sekta ya Utalii imefanikiwa kutoa fursa za ajira zisizokuwa za moja kwa moja zipatazo 60,000 na zile za moja kwa moja 22,884 ambapo takwimu zinaonyesha wazi kwamba mchango wa sekta ya utalii katika pato la Taifa umefikia asilimia 27%.
Balozi Seif alieleza kutokana na mchango mkubwa wa sekta ya utalii katika maendeleo ya Taifa Serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kitaasisi na kiutendaji ili kukidhi viwango vinavyokubalika kimataifa katika utoaji wa huduma za kitalii.
Alifahamisha kwamba Serikali itazidi kuhamasisha wananchi kuzalisha bidhaa bora na zenye viwango ambazo zitakuwa na uwezo wa kuingia kwenye soko la utalii na hivyo kuifanya sekta hii kuzidi kuwanufaisha zaidi wananchi ambao ndio walengwa wakuu.
Alieleza kuwa hivi sasa wananchi waliowengi hasa wakulima wamepata fursa ya kuuza bidhaa wanazozalisha mashambani kuuza kwenye hoteli mbali mbali hali ambayo imeongeza upatikanaji wa soko la uhakika wa bidhaa zao.
Alisema kuwa ili sekta ya utalii izidi kukuwa na kuleta tija hakuna budi kwa Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi na wananchi kuimarisha vivutio pamoja na mindombinu itakayowavutia watalii ikiwemo usafi na utunzaji wa mazingira, uwekezaji katika ujenzi wa hoteli zenye viwango bora.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliziagiza Taasisi zinazohusika katika kusimamia sekta hiyo kuandaa na kutekeleza mipango itakayoamsha ari ya wananchi kupenda kutembelea maeneo yenye vivutio vya utalii kwa lengo la kukuza utalii wa ndani.
Hata hivyo Balozi Seif alitahadharisha wazi kwamba kuimarika kwa utalii washirika wote wa sekta hiyo hawanabudi kuhakikisha kwamba mapato yatokanayo na eneo hilo yanakusanywa kikamilifu na kuingia katika mfuko Mkuu wa Serikali.
Aliendelea kusisitiza umuhimu wa kuendelea kudumishwa kwa amani iliyopo hapa nchini ambayo ndiyo kichocheo kikubwa kinachotoa fursa kwa wageni na watalii kupenda kuvitembelea visiwa vya Zanzibar.
Akizungumzia sekta ya kilimo ambayo bado ni tegemeo kubwa la wananchi waliowengi katika kujipatia ajira, kipato,chakula na kuimarisha lishe na afya zao Balozi Seif alisema Serikali inaendelea kutoa msukumo mkubwa kusaidia sekta hiyo ili wananchi waweze kuongeza tija na uzalishaji na hivyo kuimarisha vipato vyao.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Kilimo imejiandaa kikamilifu kuhakikisha kwamba huduma za kilimo cha matrekta na zana nyengine za kilimo zinapatikana kwa uhakika na kwa bei nafuu zitakazotoa nafasi kwa wakulima kuzimudu.
Alisema mpango huo utakwenda sambamba na ongezeko la kiwango cha upatikanaji wa mbegu bora ya mpunga, dawa ya kuulia magugu na mbolea kupitia programu ya ruzuku katika kilimo cha Mpunga.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitoa wito kwa wakulima wote wa zao la mpunga nchini kuungana na juhudi zinazochukuliwa na Serikali kwa kutumia fursa zilizopo kuhakikisha wanalima kwa wakati na kufuata kanuni za kilimo bora.
Halkadhalika Balozi Seif akawahimiza wakulima wote wa mazao mengine kuchukuwa juhudi stahiki kwa kufuata ushauri wa mabwana shamba na Mabibi shamba ili nao waweze kuongeza uzalishaji wa mazao yao.
Akigusia suala la udhalilishaji wa kijinsia ambalo linaendelea kuwa changamoto licha ya juhudi zinazochukuliwa za kudhibiti vitendo viovu lakini Balozi Seif alisema bado wapo watu miongoni mwa jamii wanaoendeleza vitendo hivyo.
Alisema ni wajibu wa kila mwana jamii kuzidisha mapambano dhidi ya waovu wanaohusika na matendo hayo kwa kuwafichua na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria bila ya kuwaonea muhali.
Alisema waovu hao kwa kiasi kikubwa wanavunja utu na heshima za kibinaadamu na kuwasababishia madhara makubwa ya kimwili na kiakili.
“ Watu wote wenye taarifa za waovu hao ni vyema kutosita kufika mahakamani kwa kutoa ushahidi pale wanapohitajika na kuacha kabisa masuala hayo kumalizikia majumbani “. Alisema Balozi Seif.
Kuhusu utolewaji wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwakumbusha Wananchi pamoja na Viongozi hasa wale wa Kisiasa waelewe kwamba huduma hiyo hutolewa kwa mujibu wa sheria nambari 7 ya Mwaka 2005.
Alisema muhusika lazima atimize matakwa ya sheria hiyo kabla ya kupatiwa kitambulisho ambayo ni pamoja na Mzanzibari wa kuzaliwa, mwananchi kukaa katika eneo lake si chini ya miezi 36 sambamba na kutimiza umri wa miaka 18.
Hata hivyo Balozi Seif alifafanua kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 13 { 1 } { 2 } cha sheria hiyo imetoa haki kwa mtu kukata rufaa kwa Mkurugenzi wa Vitambulisho dhidi ya Afisi ya usajili pindipo hakuridhia na mamuzi yanayotolewa au kwa waziri kama pia hakuridhika na uamuzi wa Mkurugenzi.
Alisema suala la utoaji wa vitambulisho vya Mzanzibari limekuwa na mjadala mkubwa kutokana na baadhi ya wanasiasa na waheshimiwa kulalamikia juu ya baadhi ya wananchi wao kutopatiwa vitambulisho hivyo kwa sababu mbali mbali.
Alielezea imani yake kwamba waheshimiwa wawakilishi, wanasiasa na wananchi hawana sababu ya kulalamikia suala hilo ambalo lina utaratibu mzuri uliowekwa kwa mujibu wa sheria.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitanabahisha kwamba suala zima la upatikanaji wa vitambulisho hivyo lisihusishwe na mambo ya kisiasa kwani utaratibu wa kisheria upo. Hivyo ni vyema na wajibu wa kila mwananchi kutumia sheria hiyo katika kutafuta haki yake.
Miswada Minne ya Sheria iliwasilishwa katika Mkutano huo wa 18 wa Baraza la Wawakilishi na kujadiliwa na wajumbe wa Baraza hilo ambayo ni Mswada wa sheria ya kuanzisha sheria ya kupunguza na kukabiliana na maafa Zanzibar na Mambo mengine yanayohusiana na hayo.
Mwengine ni Mswada wa sheria ya kuanzisha Taasisi ya ulinzi ya Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar, Mswada wa sheria ya kufuta sheria ya usimamizi wa mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu nambari 2 ya mwaka 1996 na kuweka badala yake msharti bora ya kuhifadhi, kulinda na kusimamia mazingira pamoja na mswada wa sheria ya maadili ya Viongozi wa umma na kuanzisha Tume ya maadili ya Viongozi na mambo mengine yanayohusiana na hayo.
Baraza la Wawakilishi Zanzibar limeahirishwa hadi Jumatano ya Tarehe 11 Machi mwaka 2015 mnamo saa 3.000 za asubuhi.
SOURCE:SUFIANIMAFOTO

Si ulinikataa Q.Chief jikumbushe na hii maisha ni safari ndefu je wewe uliwa wapi?

Sudan Kusini yatishiwa vikwazo

$
0
0
Umoja wa Afrika umetishia pande mbili zinazopigana Sudan Kusini kwamba zitawekewa vikwazo.

Baraza la Amani na Usalama la AU limesema vikwazo vitawekwa kwa pande zote ambazo zinachafua makubaliano ya amani.

Piya liliomba serikali na wapiganaji kueleza mapendekezo yao kuhusu serikali ya mpito kabla ya mkutano wa viongozi wa AU kumalizika mjini Addis Ababa.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na jumuia ya Afrika Mashariki, IGAD, piya zimetishia kuwa zitaweka vikwazo.

Mapigano yalianza mwaka 2013 baina ya wanajeshi wa Rais Salva Kiir na wale watiifu kwa makamo wake wa rais wa zamani, Riek Machar.

Mapigano yameendelea ingawa makubaliano kadha ya amani yametiwa saini.

Timu ya Simba SC, imeshinda bao 2-1 dhidi ya JKT Ruvu leo Uwanja wa Taifa, Dar.…

$
0
0

Mshambuliaji wa Simba, Danny Sserunkuma.

Mshambuliaji wa Simba, Emanuel Okwi akishangilia katika moja ya mechi ya Ligi Kuu Bara.

Timu ya Simba SC, imeshinda bao 2-1 dhidi ya JKT Ruvu leo Uwanja wa Taifa, Dar. Sasa ina pointi 16.
Mfungaji kwa upande wa Simba ni Danny Sserunkuma kipindi cha kwanza na kipindi cha pili.

MWALIMU WA KARATE NA YOGA SENSEI RUMADHA FUNDI KATIKA WARM UP !

$
0
0
Mwalimu wa michezo ya Karate na Yoga anayetambuliwa na shirikisho la kimataifa la michezo hiyo mtanzania Sensei Rumadha Fundi mwenye Black Belt na Dan 6 toka Tanzania Karate Federation( TKF), na Dan 3 toka Okinawa Goju Ryu,Japani,Sensei Rumadha Fundi ambaye makao yake yapo kule Auston,Marekani akiwa anaupasha moto mwili (warm up ) katika mazoezi yajulikanayo kama "Double Shotei Tsuki" practice.
(onyo tafadhali usijaribu kuiga au kufindisha maozezi haya mtaani au popote bila ya kuwa na utaalamu)
Viewing all 45987 articles
Browse latest View live
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>