Quantcast
Channel: VIJIMAMBO
Viewing all 45982 articles
Browse latest View live

TASWIRA YA BABY SHOWER YA NURU SIKU YA JUMAMOSI MT VERNON NEW YORK.

$
0
0
Picha ya Nuru ambayo wapendwa wake walikuwa wanaandika maneno ya pongezi kwa mama kijacho siku ya baby shower yake.
Mama kijacho Nuru jinsi alivyo pendeza akiwa amepozi kwenye kiti cha kujidai siku ya baby shower yake iliyofanya New York siku ya jumamosi, jitiririshe kwa picha na matukio ya siku hiyo kwa kuingia soma zaidi kiroho safi.


TEMBAPHOTO OFFICIAL PHOTOGRAPHER SIKU YA SHEREHE ZA CCM NEW YORK OMMY "DIMPOZ" NDIYO HABARI YA MJINI

$
0
0
 Ukumbi wa sherehe za CCM New York  tarehe 21 mwezi wa 2, Tembaphoto ndani ya mjengo kukuletea ukodak wa kiwango.

Ukiwa na shughuli yeyote inayohusu ukodak basi ni tembaphoto ndiyo suluhisho ya yote. Tembelea web site ya tembaphoto kujionea ubora wa picha.
http://tembaphoto.com/


SHUHUDIA AMANI AKILIA JUKWAANI NA MKEWE SIKU YA SHEREHE ZA THT

$
0
0
Amini Akilia jukwaani na Mkewe
Jana Jumba la Vipaji Tanzania THT walisherehekea Miaka Kumi toka Kuanzishwa Kwake Pale Escape 1, Mambo yalikuwa matamu sana kwani wasanii wote walio.....
pitia katika Jumba Hilo la Vipaji walitoa Burudani safi kabisa ya live na kufanikiwa kuwagonga nyoyo mashabiki waliofurika kushuhudia Tukio Hilo...Mpiga picha waUdaku Specially Eli Ulomi Aliweza Kupata Matukio Mbali Mbali Likiwemo la Amini na Mkewe Kulia Kwa Furaha Jukwaani , Amini na Mkewe wote ni zao la THT , walikutana Hapo na Mwisho ikazaliwa Ndoa..

HAPPY BIRTHDAY

$
0
0
Olivia Andrew wa New Jesey
Timu ya Vijimambo inakutakia kheli ya siku yako ya kuzaliwa.

Our Next Container To Tanzania Is Leaving Soon!

$
0
0
Enjoy The Game and Know That We Will Load Again End Of Feb Or Early March ( Weather Permits). Call or WhatsApp ( 240-552-4870) To Confirm & Reserve Space!

NENO LA LEO HILO

Zari Hassan kufunga ndoa na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, "Asema hakuna umri maalumu wa Kuoa au Kuolewa"!

$
0
0
WAKATI mama mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasim ‘Sandra’ akiwa nchini India kwa matibabu ya tatizo la kiafya linalodaiwa kuwa ni kupooza, hapa Bongo dalili za Diamond na mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au The Boss Lady kufunga ndoa zinanukia. 
Chanzo makini kimeliambia Ijumaa Wikienda kwamba, licha ya mama Diamond kupelekwa India Januari 27, mwaka huu na msafara wa watu wawili, nyuma, Zari alitua Bongo tangu Januari 30, mwaka huu lengo kubwa likiwa kumuuguza mama mkwe wake huyo.

ATUA DAR, AENDA SINZA-MORIChanzo kikazidi kuweka wazi kuwa mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Diamond alimpokea na kwenda naye nyumbani kwake, Sinza-Mori jijini Dar bila kumwambia kama mama yake amepelekwa India kwa matibabu.
“Diamond alikwenda kumpokea Zari lakini hakumwambia kama mama yake amekimbizwa India kwa matibabu na yeye (Zari) alikuja kwa lengo la kumuuguza mama mkwe wake,” kilisema chanzo.

BAADA YA KUMKOSA MAMA MKWEHabari zaidi zilisema kuwa, walipofika nyumbani na Zari kuambiwa mama Diamond amepelekwa India, aliumia sana na kumlaumu mpenzi wake huyo kwa nini hakumwambia kuhusu safari ya mama tangu walipokutana uwanja wa ndege.

YAISHA, DIAMOND AMPELEKA ZARI KWENYE UJENZIBaada ya kuwekana sawa kuhusu usiri wa safari ya mama’ke, Diamond alimchukua Zari na kumpeleka kwenye nyumba yake anayoijenga Mbezi-Beach, Dar kwa lengo la kumuonesha sehemu ya mali zake ambapo ilisemekana nyota huyo wa Uganda aliipenda ramani ya nyumba hiyo.

ZARI AGOMA TENA KULALA HOTELINIKatika siku za hivi karibuni, tuliwahi kuandika kuwa Zari alilala kwa mama Diamond, akapika na kupakua ambapo mawifi zake walimsifia.
Hata katika ujio wake wa Juni 30, mwaka huu, mrembo huyo mwenye utajiri mkubwa aligoma kwenda kulala hotelini na kumwambia Diamond atalala naye nyumbani kwao, Sinza-Mori.

ZARI AANZA KUBADILI DINI?Zari ni Mkristo wa Kanisa la Born Again ambalo ni la kiroho nchini Uganda. Aliingia kwenye imani hiyo baada kuokoka na kubatizwa kwa maji mengi kama Biblia inavyotaka lakini kwa kuwa na Diamond kuna dalili za kuanza kubadili imani ili kutimiza mipango ya ndoa.
“Ukiachia kwenda kwenye nyumba hiyo ya Mbezi pia Diamond ameshaanza kumfundisha Zari baadhi ya mambo ya kidini,” kilisema chanzo.

Ijumaa iliyopita ambayo kiimani, Diamond hupenda kuvaa mavazi ya Kiarabu ambayo hutafsirika ni ya Kiislam, Zari naye alitupia vazi la baibui ili kwenda sawasawa na mwandani wake huyo.

WAENDA SONGEA WOTEWakati Ijumaa Wikienda likijiandaa kwenda mitamboni, habari za moto ni safari ya Diamond kwenda mjini Songea ambapo ni makao makuu ya Mkoa wa Ruvuma.
Diamond alikwenda kwa ajili ya shoo ya sherehe za Chama cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 38 tangu kuasisiwa kwake. Sherehe hizo zilifanyika kwenye Uwanja wa Majimaji jana.

ZARI KWAPANIHabari za uhakika ni kwamba, katika safari hiyo, Diamond alimuweka Zari kwapani na kwenda naye kwa lengo la kumpa kampani.

DIAMOND: KILA KITU KINA WAKATI WAKEIjumaa Wikienda lilimtafuta Diamond kwa njia ya simu ambapo awali alikiri mama yake kupelekwa India kwa matibabu. Kuhusu Zari kubadili dini, kuvaa hijabu na kufunga ndoa, alisema: “Mbona mna maswali sana jamani, kila kitu kina wakati wake.”

BREAKING NEEEEEEWWZZZZ -RIDHIWANI KIKWETE NDIO MGENI RASMI BIRTHDAY BASHH YA CCM NEW YORK FEB 21

$
0
0
             JE NI MSANII GANI ATAKAYE WARUSHA ROHO KWENYE BIRTHDAY BASHH YA CCM NEW YORK FEB 21?????..                     

""AIN'T NO PARTY LIKE A NEW YORK PARTY""
                                                   Tuungane Tuiline Tanzania Yetu



                          

                                         UKUMBI WA RICHI RICH PALACE KWA NJE                          
                                     UKUMBI UNAVYOONEKANA KWA NDANI
                          
                                                  TICKETS PRICE: ADVANCE $40 | DOOR $50
Inclusive of:
*Red Carpet Grand Entrance
*Photo up Dress Ready
*3-Course Dinner
*Soft Drinks
*Elegant Settings
*Live Entertainment
*Cash - Bar Beer $3| Liqour $5 | Wine $5 | Patron $7
CALL: 347-663-0781  | 917-698-6943 


WARIZI WA UJENZI AKAGUA BARABARA MBEYA NA RUKWA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wakazi wa mji wa Tunduma mkoani Mbeya kuwa Serikali itajenga barabara ya njia nne katika mji huo ili kupunguza msongamano wa magari na kuuwezesha mji huo kuwa wa kisasa na kibiashara.
Amesema hayo katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya barabara inayoendelea katika mikoa ya Mbeya na Rukwa ambapo akiwa mjini Tunduma amekutana na wananchi wanaofanyabiashara katika mji huo.
“Dumisheni umoja,amani na mshikamano ili mfanye biashara zenu na kukuza uchumi nasi tutahakikisha tunajenga barabara ya njia nne ili kupunguza msongamano wa magari na kuuwezesha mji wa Tunduma kuwa wa kisasa na kibiashara na hivyo kuwa mahali pazuri pa watu kuishi”,amefafanua waziri Magufuli.
Katika ziara hiyo waziri Magufuli amekagua mizani ya Nkangamo na barabara ya Tunduma –Sumbawanga KM 225, iliyojengwa kwa kiwango cha lami na kuwataka wananchi wa mkoa wa Rukwa kutumia barabara hiyo kukuza uchumi wao na wa mkoa wao kwa kufanyakazi kwa bidii.

Akihutunbia wananchi wa Sumbawanga Waziri Dkt. Magufuli amewataka wananchi kutambua kuwa barabara za lami zinajengwa kwa gharama kubwa hivyo wazitumie kwa manufaa na wale walioko kwenye hifadhi ya barabara wabomoe nyumba zao mapema ili kuwezesha ujenzi kufanyika kwa wakati.
Waziri Magufuli amesema Serikali iko katika hatua za awali kujenga barabara ya Matai-Kasesha KM 50 kwa kiwango cha lami ili kuunganisha mkoa wa Rukwa nan chi ya Zambia na hivyo kuvutia wawekezaji wengi kuwekeza mjini Sumbawanga na hivyo kutoa fursa za ajira na uchumi kwa wananchi.
Waziri Magufuli yuko katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya barabara katika mikoa ya Mbeya,Rukwa,Katavi na Tabora ambako kuna miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara za lami inayoendelea.
MWISHO.
Imetayarishwa na kitSengo cha habari na mawasiliano serikalini wizara ya ujenzi.

Barua-Bushoke jikumbushe na hii inaweza kukurudisha kumbukumbu zake za safai ndefu ya maisha haya

SINGLE MPYA YA AY- ZIGO JIPAKULIE HAPA CHINI KIROHO SAFI

Milioni 100 zaiua Yanga U/Taifa

$
0
0

Wachezaji wa Yanga (kijani na njano) wakichakarika mbele ya wapinzani wao, Ndanda FC, katika mechi ya ligi kuu bara kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jana Jumapili. 
By Khatimu Naheka 
Timu hiyo ambayo imesajili wachezaji wengi chipukizi na wasio na uzoefu, imewahi kukanya Dar es Salaam mara moja tu lakini walipofika kwenye Stand Kuu ya Mabasi Ubungo wakaonyeshwa uelekeo wa Mbagala ambako walikwenda kucheza na JKT Ruvu na walipotoka wakapitiliza kwao Mtwara wakabaki kuusikia tu Uwanja wa Taifa kwenye redio na magazeti.
NDANDA FC ya Mtwara imeweka rekodi ya aina yake kwa kukanyaga kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam na kulazimisha suluhu na Yanga ambayo usajili wake ni zaidi ya Sh500 milioni.

Timu hiyo ambayo imesajili wachezaji wengi chipukizi na wasio na uzoefu, imewahi kukanya Dar es Salaam mara moja tu lakini walipofika kwenye Stand Kuu ya Mabasi Ubungo wakaonyeshwa uelekeo wa Mbagala ambako walikwenda kucheza na JKT Ruvu na walipotoka wakapitiliza kwao Mtwara wakabaki kuusikia tu Uwanja wa Taifa kwenye redio na magazeti.

Lakini jana Jumapili kwa mara ya kwanza wametoa ushamba baada ya kuingia na kucheza kwenye uwanja huo wakiwa na usajili wao wa Sh100 milioni ambao uliizuia Yanga yenye wachezaji watano wa kigeni na Kocha Mholanzi Hans Pluijm.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Ndanda ambao jana walikuwa wakishangilia kana kwamba wametwaa ubingwa, Edmund Kunyengana, alithibitisha kwamba kwenye usajili mkubwa walitumia Sh80 milioni na dirisha dogo Sh20 milioni.

Katika mchezo wa jana, Yanga ikitumia mastraika wake mahiri; Kpah Sherman, Amissi Tambwe, Mrisho Ngassa, Jerry Tegete na Danny Mrwanda ilikosa mabao manne ya wazi kitendo ambacho kilimkera kocha Pluijm.

Pluijm alisema: “Tumekosa mabao manne ya wazi na kama wangekuwa makini tungepata ushindi kabisa, kila mtu ameona.” Matokeo hayo yameifanya Yanga sasa kuwa na pointi 19 ikishikilia nafasi ya pili huku Ndanda ikiwa na pointi 14. Katika kipindi cha kwanza Yanga ilifanya mashambulizi matano ya maana langoni kwa Ndanda kupitia kwa Msuva, Ngassa, Mrwanda na Nadir Haroub ‘Cannavaro’, lakini kipa wa zamani wa Simba, Wilbert Mweta aliyazuia na mengine yakapaa.

Ndanda ambao walikuwa wakishangiliwa na mashabiki wa Simba, walikuwa na mashambulizi mawili ya maana kupitia kwa fowadi wake Masoud huku Omega Seme akionyesha ufundi wake kuituliza Yanga.

Kipindi cha pili Yanga ilionekana kujipanga lakini Ndanda wakatumia akili za ziada kwa kujiangusha mara kwa mara pamoja na kucheza na saikolojia za wachezaji wa Yanga ambao walionekana kama wamepaniki.

Dakika ya 90 mwamuzi Martin Saanya wa Morogoro alimwonyesha kadi nyekundu, Ernest Mwalupani, wa Ndanda ikiwa ni kadi yake ya pili ya njano kwenye mchezo huo ambao mashabiki wa Yanga walikuwa wakipaza sauti nje ya uwanja wakitishia kutokuja uwanjani tena huku wenzao wa Simba wakiwakejeli kwamba “Mmewashindwa hata Ndanda ambao tumewapiga, mwaka huu mnalo.”

Kocha wa Ndanda Abdul Ngange alisema walitua Dar es Salaam wakiwa wanajua mazingira ya uwanja na mchezo utakavyokuwa hivyo akawaambia wachezaji wake wakabe mpaka kivuli kuanzia sekunde ya kwanza mpaka ya mwisho jambo ambalo walifanikiwa.

Ndanda; Wilbert Mweta, Aziz Sibo, Paul Ngalema/Shukuru Chachala, Kasian Ponela, Ernest Mwalupani, Zablon Raymond/Hemed Khoja, Jacob Massawe, Omega Seme, Nassoro Kapama, Stamili Mbonde, Masoud Ally/Isihaka

Yanga; Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Rajab Zahir, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Salum Telela, Simon Msuva, Hassan Dilunga/Said Makapu, Kpah Sherman/Amissi Tambwe, Danny Mrwanda,Mrisho Ngassa/Jerry Tegete. Katika mchezo mwingine jana, Ruvu Shooting iliishinda Stand United mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Mabatini mabao yakifungwa na Juma Mpakala na Yahya Tumbo. Hamis Thabit alifunga bao la Stand.
SOURCE:MWANASPOTI

PAZI BASKETBALL REUNION COMING IN HOUSTON

$
0
0

MARCH 14,2015 MORE INFORMATION COMING SOON!!!

Kali TV at the Washington DC Auto Show

[Diamond]Mpenzi Wangu Mjamzito Kweli

$
0
0

Mwanamuziki maarufu nchini na sehemu nyingi za dunia – Diamond Platnumz ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa mwanadada Wema Sepetu ameendelea kuuhakikishia ulimwengu kuwa, mpenzi wake wa sasa ZARI al-maarufu kama “The boss lady”, ni mama mtarajiwa aliyebeba ujauzito wa msanii huyo nguli nchini na kwamba hii sio project nyingine.

Huku akitumia mafumbo kwenye maneno yake ambayo wataalamu wetu wa Kiswahili ndio wametufafanulia kisanifu zaidi, Diamond aliandika

“Kileeeeeeee kinaanza kumuharibia mtu Mavazi..”huku akiweka picha yake na mpenzi wake huyo wakitoka kwenye show ya miaka 38 ya CCM huko songea. Baada ya kukaa chini vizuri na wataalamu wetu hawa wa fasihi , walituhakikishia kuwa “Kileeeee” katika sentensi hiyo sio kitu kingine bali ni ujauzito alionao mrembo huyo na mara nyingi ukichunguza ndio kitu kinachomuharibia mwanadada au yoyote mavazi kirahisi hasa “kinapoanza” kuwa kikubwa.Kweli tumeamini lazima ujue tofauti ya msalaba na kujumlisha.
SOURCE:SHAFFIHDAUDA


NGONO ZEMBE YATAWALA HIKI KIJIJI, INA MAANA HAWAOGOPI HUKIMWI?

$
0
0

Hii ndio hali halisi utakayo kutana nayo kilometa 660 kutoka Dar es Salaam na kilimeta 122 kutoka Nachingwea. 

Katika kijiji cha Kiegei kila tarehe 25 ya mwisho wa mwezi, baada ya mnada wa bidhaa mbalimbali za kilimo kama chakula na vifaa vya nyumbani kama vyombo.

Watu wengine, wekiwemo watoto wa shule za msingi huuziana mabusu na wafanyabiashara wa mnada huo, kusababisha kukatisha masomo kwa baadhi ya wanafunzi kwa kushika ujauzito na wengine kupata magonjwa ya kuambukiza kama gono, kaswende na Ukimwi.

Baada ya kuuza bishaa zao mbalimbali katika mnada huo, unaohusisha wafanyabiashara kutoka katika wilaya za jirani kama Liwale, Tunduru na Masasi, wafanyabiasha wa Kiegei huingia katika vibanda vya sinema, mathalani kuangalia filamu mbalimbali, lakini humo ndani ya vibanda filamu hutumia pesa zao kununua ngono kutoka kwa watoto.

Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 inalenga kuhakikisha kwamba watoto wote wanastawi na kuwa na maisha bora, kutokana na kupatikana kwa haki zao za msingi ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kulindwa na kushirikishwa katika mambo yanayowahusu bila ua ubaguzi wa hali yoyote. 

Kwa mujibu wa sera hiyo, mtoto ni yule mwenye umri wa chini ya miaka 18. Mtu yeyote mwenye umri wa chini ya miaka 18 anastahili kulindwa na familia yake pamoja na wanajamii wanaomzunguka ili kumuangalia ukuaji wake uwe wenye usalama zaidi.

Madhara ambayo anaweza kuyapata mtoto kama hajapata uwangalizi kutoka katika familia yake na jamii inayomzunguka ni, kuathirika kiafya, kiakili, kimwili, kihisia na kijinsia. 

Pia pale ambapo maendeleo ya mtoto yanavurungwa, ni pale uhai wa mtoto uko hatarini pamoja na utu wa mtoto unapokosekana.

Sheria ya kimataifa ya mwaka 2009 ya kutetea watoto kutoka umoja wa mataifa inaeleza kuwa, mtoto wa chini umri wa miaka 18 anatambulika kama mtoto kidunia na anastahili kulindwa na familia yake na kupewa mahitaji muhimu kama chakula bora, maradhi, nguo na elimu bora, mtoto huyu atakiwa kuanza kujitegemea yeye mwenyewe au kuachiwa huru kufanya ngono zembe na ajira majumbani na mashambani ili alishe familia hairuhusiwi kimataifa.

Lakini, ukitembelea vibanda vya sinema vya kijiji cha Kiegei kuanzia saa 12.00 jioni, utawakuta watoto wa kike, wenye umri kuanzia 10 hadi 14, katika shuguli mbali mbali za kutafuta hela kwa kuuza ngono.
Siku ya tarehe 25 Januari, 2013, ambayo ilikuwa ni siku ya ijumaa, zikioneshwa sinema za kivita mbili, wasichana wapatao 10 walionekana ndani ya kibanda cha sinema kilichopo katika kijiji cha Kiegei, wakipakwatwa na kushikwa-shikwa na wanaume wenye umri mkubwa.

Saa 6:00 usiku, kila mtoto alitoka na mwanaume na kuelekea sehemu mbalimbali kama vyoo vya shule ya msingi Kiegei, uwanja wa mpira na wengine kwenye meza za mchezo wa pool, iliyopo katika Soko dogo la kijiji cha Kiegei na wengine pembezoni mwa jengo la Kanisa.

Mtoto huyo na mwanaume mtu mzima wakiwa katika meza ya mchezo wa pool, wakaanza kufanya ngono mbele ya macho yangu, bila hata ya kuona aibu yoyote, tena bila hata huruma kama anayefanya naye ngono ni mtoto wa shule ya msingi.
“Kama unaona mwenzio anafaidi na tendo hili la ngono basi njoo weye mtu mzima ufanye;naona umeshangaa kwa kutoa macho utazani hujui nini kinachofanyika hapa,” alisema jibaba hilo huku akiendelea kufanya ngono na kitoto hicho. 

Saa 12:00 asubuhi kesho yake, hakukukuwa na mabaki ya kondom katika maeneo haya yote. 

Kwa mujibu wa wanafunzi wa shule ya msingi Kiegei, wanalipwa kiasi cha sh.500 hadi sh.2000 kufanya ngono na watu wazima.

“Nimeanza ngono nikiwa na umri wa miaka 12, kabla hata sijabalehe nafanya ngono na wanaume wakubwa ambao ni wachimbaji wa madini Mbwemkuru na wafanyabiasha ya mnada wanaofika kila tarehe 25 ya mwisho wa mwezi, kwa ujila wa Tshs. 500 hadi Tshs. 2000 kwa siku,” alisema Anna Peter (13) sio jina lake

Wakati huo huo, mwalimu mkuu wa shule ya Kiegei, Fred Mchekenje, alisema kuwa wanafunzi wa shule yake bado hawajaanza kufanya ngono kwani bado wadogo sana na kudai kwamba mambo hayo wanafanya watoto wa mitaani.
“Bado wadogo sana; hawajaanza kufanya mambo hayo ya kiutu uzima. Wanapenda kusoma na muda mwingi wako nyumbani wanajisomea wakitoka shuleni,” alisema Mchekenje. 

Mchekenje alisema kuwa, mwaka 2012 wanafunzi wapatao 29, walifanya mtihani wa kumaliza darasa la saba, kati ya hao wanafunzi 29 walifaulu kujiunga na kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Kiegei, kati ya hao wasichana 11 na wavulana 18.

Mwaka 2011 wanafunzi walifaulu walikuwa asilimia 70 na wakapata fulsa ya kujiunga na masoma ya sekondari na vyuo vya ufundi stadi veta.

Asilimia 30 ndio waliobaki mtaani ambao hawakufaulu na kupata nafasi ya kuendelea na masomo ya sekondari katika shule mbalimbali za sekondari Nachingwea.

Aidha alisema kuwa matokeo ya darasa la nne yalikuwa mabaya sana kwa mwaka 2012; waliofanya mtihani walikuwa 95 na waliofaulu ni watoto nane tu. Kati ya hao, wavulana walikuwa sita na wasicha ni wawili. Kwa mujibu wake, sababu kubwa ya kufeli ni kutokuwepo kwa vitabu, chaki na upungufu wa walimu; badala ya 15, kwa sasa wapo watatu.

Mchekenje alisema kuwa mahudhurio ya watoto wa kike shuleni ni mazuri na hakuna mimba iliyopatikana kwa miaka saba sasa; mara ya mwisho kumpata mtoto mwenye ujauzito ni mwaka 2006. Anadhani sababu kubwa ya kupungua kwa mimba shuleni ni kuwepo kwa somo la elimu lika lililoanza kufundishwa mwaka 2007.

Kwa mujibu wa Juma Ramadhani, ambaye ni mkazi wa kijiji hicho na mzazi wa watoto watatu wanasoma katika shule ya msingi Kiegei, mwaka 2012, wanafunzi wawili walipata mimba wakiwa darasa la sita na kukatisha masomo yao.

Kama Anna, Salima Musa (sio jina lake) ni mwanafunzi wa shule ya msingi. Mtoto huyu, amabye ana miaka 11 na yuko darasa la tano katika shule ya msingi Ukombozi anasema, “Nimezoeya kufanya ngono na watu wazima. Sitaki watoto wa shule wenzangu kwa sababu wananuka mkojo; nataka wanaume wenye misuri iliyokomaa kwani ndio nasikia raha zaidi.” 

Aziza Ally (siyo jina lake) aliacha shule mwaka huu, akiwa darasa la sita. Hana ndoto tena za kwenda shule maana ngono anayofanya ndio inampa uwezo wakuilisha familia yake kwa sasa.

“Sijawahi kutumia kondom toka nimeanza kufanya ngono nikiwa darasa la nne. Kwa sasa nimeamua kuacha shule kwa sababu walimu wameniamba nirudie darasa la tano badala ya kuwa darasa la sita. 

Nimeona bora nifanye ngono ili nijikimu kimaisha kwa kujinunulia nguo, viatu na mafuta mazuri pamona na kutoa nyumbani pesa ya chakula. Hapa unaponiona nimetoka kumaliza dozi ya ugonjwa wa gono wiki moja iliyoisha na sasa niko mawindoni natafuta pesa.” 
Baba yake Aziza aliki kufahamu kwamba mtoto wake anajihusisha na ngono zembe.

“Nimemkanya asifanye ngono lakini hasikii. Nimeamua kumuacha tuu ila kwa sasa sina huduma yoyote ninayopa mtoto huyo; anajinunulia mwenyewe nguo za kuvaa, mafuta ya kupaka na chakula,”alisema Baba yake Aziza.


Kwa mujibu wa Dk. Kahabi Isangura, mtaalamu wa magonjwa ya kijamii, kuna madhara makubwa sana kwa mtoto kuanza kufanya ngono katika umri mdogo. Anaweza kupata mimba na kukatisha ndoto zake za kusoma, anaonekana muhuni pamoja na kukabiliwa na majukumu makubwa akiwa na umri mdogo.

Dk. Isangura alisema kuwa madhala ya kiafya ni kama kupata magonjwa ya kuambukiza yakiwemo ukimwi, gono, kaswende na kisonono. Pia, anaweza kupata kansa ya kizazi kwa kuanza ngono mapema kwa sababu seli za kingo za uke zinakuwa hazijakomaa vema, hivyo nirahisi kupata majereha na kuweka ufa ambao unasababisha kupata kansa ya kizazi akiwa mtu mzima.

Ngono ya utotoni husababisha vifo vya wajawazito wakati wa kujifungua kwa sababu mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 14 nyonga yake ya uzazi inakuwa bado haijakomaa kusukuma mtoto wakati wa kujifungua, hivyo basi kunauwezekano mkubwa wa mtoto huyu kupoteza maisha wakati wa kujifungua.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Mganga wa Zahanati ya Kiegei Olafu Chinguile, mwaka 2011 wagonjwa 48 walifika wakiwa wanaumwa magonjwa ya Kaswende na Gono; kati ya hao watoto walikuwa 5.
Mwaka 2012 wagonjwa waliofika katika zahanati yake wakiwa wanaumwa magonjwa ya Gono na Kaswende walikuwa 38; kati ya hao, nane walikuwa watoto kati ya miaka 10 na 14.

Habiba Juma alimaliza darasa la saba katika shule ya msingi kiegei mwaka 1994 na kusema kuwa, kipindi alichokuwa anasoma yeye hakukuwa na mambo ya ngono kwa wanafunzi na watu wazima, lakini ilipofika mwaka 1995 ndio mambo ya ngono kwa wanafunzi yalipoanzia baada ya kuanza kwa machimbo ya madini.
Makwasa Bulenga ni Afisa elimu wa shule ya msingi wilaya ya Nachingwea alisema kuwa,tatizo kubwa la wanafunzi kufanya ngono ni kuwepo kwa vibanda vya kuonesha sinema mbalimbali muda wa usiku.


“Vibanda vya sinema kwa vijijini ndio tatizo kubwa kwa watoto wa shule ya msingi kujifunza mambo machafu, huku sinema hizo wakiangalia na watu wazima tena wanaume hasa wachimbaji wa kutoka sehemu mbalimbali za uchimbaji,”alisema Bulenga


Bulenga alisema kuwa ofisi yake imewaita mara kadhaa viongozi wa vitongoji na vijiji kuwaeleza umuhimu wa vibanda vya sinema kufungwa mapema, lakini juhudi hizo zimegonga mwamba kwa sababu vibanda hivyo vinaanza kuonesha sinema kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 6:00 usiku na wateja wao wakubwa ni watoto wa shule za msingi.
Vibanda vya sinema vinatakiwa kuanza kuonesha sinema saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni.


“Sio tuu kiegei watoto kufanya ngono; na vijiji vingine pia hali ni hiyo hiyo kama uliyoishudia kiegei, bado tupo katika hali mbaya sana kwa watoto kuanza ngono mapema kwa wilaya ya Nachingwea,” alisema Bulenga.


Kwa mujibu wa Bulenga, katika wilaya ya Nachingwea kuna kata 32; kati ya hizo, kata sita pekee ziko mjini. Nyingine zote ziko vijijini na sehemu kubwa yake ndio kuna wanafunzi wengi ambao wanafanya ngono baada ya kumaliza kuangalia sinema za ngono katika maeneo hayo.


Mjini kuna wanafunzi wapatao 4,789; wavulana ni 2,365 na wasichana 2,424. Vijijini kuna wanafunzi 27,047; kati yao, wavulana wako 13,319 na wasichana ni 13,728. Walimu waliopata mafunzo kuhusu somo la elimu lika kwa wilaya ya Nachingwea wako 23; wanaume 14 na wanawake9.


Inapaswa kuwa na walimu ambao wamepatiwa elimu lika 300, ili kiweza kukidhi idadi ya wanafunzi wa shule za mjini na vijijini katika wilaya ya Nachingwea kwa sasa.


Walimu ambao hawakupata mafunzo lakini wanafundisha somo hilo la elimu lika wako 200; wanaume 116 na wanawake 84. Hii inachangia uwajibikaji mdogo kwa walimu ambao hawajapatiwa mafunzo ya somo hilo jinsi ya kumfundisha mwanafunzi akajiepusha na ngono.


Kwa upande wake, Jane Mrema mshauri wa masuala ya jinsia na kutetea haki za watoto na vijana kutoka Plan International alisema kuwa, tatizo la shule ya msingi Kiegei kwa watoto kuanza ngono halifahamu. 


Mrema alisema kuwa watoto wanalengwa na shirika la Plan International ni kuanzaia mwezi mmoja mpaka miaka 18, hasa kwa watoto wa kike pamoja na walemavu. Kwa sasa wanafanya kazi katika mikoa mitano nayo ni Mwanza, Geita, Morogoro, Pwani na Dar es salaam lakini pia wanafanya katika wilaya sita ambazo ni Kibaha, Kisarawe, Kilombero, Sengerema, Ilemela, Geita na Ilala. 


“Tunamuelisha mtoto wa kike kutambua haki yake ya kupata elimu bora na afya bora, pia mtoto kufahamu unyanyasaji wa kijinsia majumbani na njiani akienda shuleni, pamoja na kuangalia mazingira ambayo yapo hatarishi kwa kupata unyanyasaji wa kijinsia kwa mtoto wa kike,” alisema Mrema.


Aidha Plan International wamejenga mabweni katika wilaya mbalimbali kama Ilala katika shule ya sekondari sakara, kibaha shule ya sekondari ya ruvu, mwanza na geita kila bweni linauwezo kuchukua watoto 100, pia wamejanga choo na mabomba ya maji safi.


Kwa sasa kuna kampeni nyingine ijulikanayo kama kwa sababu mimi ni msichana ambayo lizinduliwa mwishoni mwezi wa Octoba mwaka jana, lengo kubwa la kampeni hii ni, kuhamasisha jamii kutetea haki za mtoto wa kike kwa sababu watoto wa kike ndio waathirika wakubwa.
Kampeni hii ilikuwa na ujumbe usemao maisha yangu, haki yangu tokomeza ndoa za utotoni, kampeni hii hasa inajikita kumtetea mtoto wa kike kuepukana na unyanyasaji wa kijinsi na kupata haki zake za msingi na elimu bora.



Pia wamejikita katika suala la afya ya uzazi kwa watoto wa kike, kwa kuwajengea uwezo kujilinda na kujitunza na kufikia ujana vizuri, pia kutokomeza mira potofu kama ukeketaji na ndoa za utotoni.

TRADE WINDS MISSION TO AFRICA- EVENT FEBRUARY 3, 2015

$
0
0
U.S. commercial Service - Trade Winds - Africa
After-Hours Networking Series
Date: Tuesday, February 3, 2015
Time: 6:00 to 8:00 p.m.

Topic: Trade Winds Africa – U.S. Africa Trade
Location: Embassy of Ethiopia, 3506 International Drive, NW, Washington,
DC 20008 (Note: Parking is limited)
Metro Stop: Van Ness UDC (Red Line)

H.E. Ambassador Girma Birru of Ethiopia along with Their Excellencies
Ambassador Robinson Njeru Githae of Kenya and Ambassador Liberata Mulamula
of Tanzania, and The Virginia – Washington, DC District Export Council
(DEC), cordially invite you to a networking reception at the Embassy of
Ethiopia on Tuesday, February 3rd from 6 to 8 PM.

This event will give you the opportunity to network with U.S. trade
officials and members of the African diplomatic community, and to hear the
latest opportunities and momentum around U.S.-Africa trade including
important announcements about Trade Winds Africa, the largest ever U.S.
government-led trade mission to Africa.
http://trade.gov/dbia/tradewinds-africa/index.asp

Due to Embassy security, pre-registration is required for each attendee
and is non-transferable. Admission to the event will not be granted to
attendees or their guests who have not pre-registered. If you bring a
guest you MUST register them. Also note that parking is limited so please
plan accordingly. The nearest Metro stop is Van Ness-UDC which is several
blocks from the embassy.

There is no cost to attend.

Inquiries:
Please e-mail Olga.Ford@trade.gov. Via phone Olga can be reached at
703-235-0070 Additional inquiries: info@isi-consultants.com

Please proceed with online registration below.

http://www.isi-consultants.com/dec-networking-series

Kindest regards
Paul Mwafongo

DKT. NCHIMBI ASEMA CCM HAINA TATIZO LA KIMUUNDO WALA MFUMO

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza katika maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, yaliyofanyika kitaifa juzi kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea, Mkoani Ruvuma.Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa maandalizi ya sherehe za maika 38 ya Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni mbunge wa Songea mjini Dkt Emmanuel Nchimbi amesema kuwa chama chake kina kila sababu ya kushinda kwa kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa kuwa kina mfumo na muundo imara.

Akizungumza muda mfupi baada ya maadhimisho hayo mjini Songea, Dkt Nchimbi ambaye pia ni mjumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho alisema kuwa chama chake hakina tatizo la kimfumo wa muundo na kuongeza kuwa ushindi ni lazima.

“Chama hakina tatizo la muundo wala mfumo na tutakachofanya ni kubadilisha mikakati tu ili kujihakikishia ushindi katika uchaguzi ujao,” alisema
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe katika maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, yaliyofanyika kitaifa juzi kwenye Uwanja wa Maji Maji mjini Songea, Mkoani Ruvuma katikati ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho.

Aliongeza, “Kwa kwa kaida hakuna mkakati unadumu. Mar a zote mikakati hubadilika kulingana na mazingira na hiki ndicho tutakachokifanya,”

Akizungumzia kuhusu kauli ya mwenyekiti wa chama hicho Rais Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa chama kuwatembelea wanachama na kushawishi wanachama wapya, alisema CCM ni chama kikubwa na ndani yake wapo viongozi waliolala ambao mwenyekiti wa taifa aliwakumbusha kuamka na kufanya kazi.

“Chama hakiwezi kuwa na maisha marefu kama viongozi katika ngazi zote ha hawajitumi. Katika jeshi kubwa kama hili la CCM wapo watu ambao lazima wasukumwe na ndiyo ahwa mwenyekiti wetu wataifa aliwasukuma kupitia hotuba yake.

Hawa wanatakiwa kuamka na kuanza kufanya kazi kwa bidii ili kukiwezesha chama kushinda kwa kishindo kama ambavyo kimekuwa kikishinda tangu kuanza kwa siasa za vyama vingi,” alieleza
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea, Dk. Emmanuel Nchimbi (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Dkt Nchimbi aliishukuru halmashauri kuu ya chama kwa kuweza kuuchagua mkoa wa Ruvuma kwa ajili ya maazimisho ya miaka 38 ya chama hicho na kueleza kuwa kwa miaka mingi Ruvuma imekuwa ngome imara ya CCM.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho alisema kuwa alisema kuwa chama chake kimeshaanza kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu .

“Nimeshawaagiza viongozi wa chama katika ngazi ya mkoa na wilaya kuanza vikao kwa ajili ya na kuweka mikakati thabiti ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao,”

Alieeleza kuwa, chama katika mkoa wake tayari kilishaanza mikakati ya kujitegemeza ikiwa ni kufuata agizo la mwenyekiti wa taifa ambapo tayari kimejipanga vyema kuendeleza vyanzo vyake vya mapato pamoja na kuanzisha vyanzo vipya kwa ajili ya kukifanya kujitegemea.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea, Dk. Emmanuel Nchimbi (kulia) akijadiliana jambo na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula (katikati) pamoja na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana.

Mhe. Rais Kikwete ampokea rasmi Rais Gauck-Ikulu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimpokea rasmi Rais wa Ujerumani, Mhe. Joachim Gauck katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais Kikwete akiwa ameongozana na mgeni wake Rais Gauck mara baada ya kumpokea. 
Rais Kikwete na Rais Gauck wakipata heshima ya nyimbo za mataifa yao ikiwa ni sehemu ya mapokezi ya Rais Gauck. 
Kikosi cha jeshi kikipiga mizinga 21 kwa heshima ya Rais Gauck 
Rais Gauck akikagua Gwaride la Heshima 
Sehemu ya waandishi wa Habari wakiwa kazini 
Sehemu ya umati wa watu waliofika Ikulu kwa ajili ya mapokezi ya Rais Gauck 
Rais Gauck akisalimiana kwa furaha na wanafunzi waliofika Ikulu kumpokea 
Picha ya pamoja 
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mama Schadt, Mke wa Rais wa Ujerumani 
Mhe. Rais Kikwete akimpatia Rais wa Ujerumani, Mhe. Gauck zawadi ya picha ya michoro maarufu nchini ya "Tingatinga" 
Rais Kikwete akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na Rais Gauck 
Rais Kikwete na Ujumbe wake wakiwa kwenye mazungumzo rasmi na Mhe. Gauck na Ujumbe wake (hawapo pichani) Kulia kwa Rais ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Memnbe (Mb.). Wengine ni Prof. Jumanne Maghembe (wa tano kushoto) , Waziri wa Maji. 
Rais Gauck (wa tano kulia) na Ujumbe wake wakati wa mazungumzo rasmi 
Mazungumzo yakiendelea 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kushoto) akiwa na Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo rasmi kati ya Rais Kikwete na Rais Gauck (hawapo pichani) Picha na Reginald Philip.

Rais wa Ujerumani awasili nchini kuanza ziara ya kitaifa

$
0
0
Rais wa Ujerumani, Mhe. Joachim Gauck pamoja na Mhe. Mama Schadt wakiteremka kwenye ndege mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku tano hapa nchini. 
Mhe. Gauck akilakiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mohammed Gharib Bilal mara baada ya kuwasili nchini. 
Mhe. Gauck na Mama Schadt wakipokea maua kutoka kwa Watoto Elizabeth Jackson na Barqat Mvungi walioandaliwa kwa ajili ya mapokezi yake. 
Mhe. Gauck akiongozana na Mhe. Dkt. Bilal 
Mhe. Gauck na Mama Schadt kwa pamoja na Mhe. Dkt. Bilal na Mkewe Mama Asha Bilal wakifurahia burudani ya ngoma wakati wa mapokezi yake. 
Baadhi ya wakina mama wa Dar es Salaam waliofika kumpokea Rais Gauck wakipeperusha bendera ya Tanzania na Ujerumani kwa furaha 
Mhe. Rais Gauck akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine wakati wa mapokezi. 
Mhe. Rais Gauck akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Philip Marmo wakati wa mapokezi yake. 
Mhe. Gauck akifurahia jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Victoria Mwakasege aliyekuwepo uwanjani hapo kwa mapokezi. 
Rais Gauck akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Bw. Assah Mwambene 
Picha na Reginald Philip.
Viewing all 45982 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>